SUAMEDIA

Fanyeni kazi kwa kufuata taratibu, kanuni na sheria ili chuo kifikie malengo yake - Prof. Chibunda

Vedasto George

SUA

Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine Cha Kilimo (SUA) Prof. Raphael Chibunda amewataka wafanyakazi kufanya kazi kwa kufuata taratibu, kanuni na sheria za kiutumishi ili chuo hicho kiweze kufikia malengo yaliyowekwa.


Prof. Chibunda akihutubia wafanyakazi wa SUA siku ya Mei Mosi

Prof. Chibunda ametoa wito huo wakati akitoa hotuba yake kwenye   siku ya maadhimisho ya siku ya wafanyakazi kwenye ukumbi wa chuo wa Multipurpose ambapo amesema kuwa njia pekee ambayo inaweza kupelekea chuo kufikia malengo yake ni wafanyakazi kuakikisha wanafanya kazi  kwa bidii pasipo kuwa na uzembe wa aina yeyote.

 “Nitoe wito kwa wafanyakazi wote, tufanye kazi kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu na uadilifu  mkubwa, hili suala la uadilifu muda mwingine lina changamoto zake ninafahamu  bado hapa chuoni kuna vitengo vyetu ambavyo vinatuumiza  zaidi sisi wenyewe  lakini vingine vinakiumiza chuo chetu  na hasa wadau wetu wa nje,  kuna malalamiko makubwa mfano kwa wenzetu kitengo cha Ununuzi  kuna ucheleweshaji, ununuzi wa vitu ambavyo bei yake inaitia hasara serikali kupitia chuo  lakini bado kuna malalamiko ya matumizi ya lugha chafu kwa watu. Amesema Prof.Chibunda.


Mmoja wa wafanyakazi bora akipokea cheti kutoka kwa Makamu Mkuu wa Chuo

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi RAAWU tawi la SUA Faraja Kamendu amesema siku ya wafanya kazi duniani  ni siku ambayo inatumiwa kwa ajili ya ukumbusho  wa mafanikio ya kijamii na kiuchumi  ikiwa ni matokeo  chanya yaliyoletwa na vuguvugu la wafanyakazi  lililotokea karne ya 18.

Kamendu ameuomba uongozi na menejimenti ya chuo kuharakisha mchakato wa kuwapatia mafao baadhi ya watumishi waliopoteza sifa ya utumishi na  kuondolewa kazi  baada  kukosa sifa ya elimu ya kidato cha nne  hasa wale ambao waliajiriwa  baada ya waraka wa serikali wa mei 4 mwaka 20004.


Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi RAAWU tawi la SUA Faraja Kamendu akizungumza katika sherehe ya wafanyakazi SUA

“Watu hawa tunajua waliitetea SUA na waliisaidia  kwa sehemu kubwa  na watu hawa waliandika barua angalau kuomba  kama kuna kitu chochote wanaweza wakapata  hasa kwenye mifuko yao ya kijamii” Amesema Kahedu

Naye Kaimu Katibu wa Chama cha Wafanyakazi RAAWU tawi la SUA Farida Mkongwe Kurunge wakati akisoma risala ya wafanyakazi wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA  mbele ya Makamu wa Mkuu wa Chuo hicho amesema ili wafanyakazi waweze kuwa na mshikamano imara ni lazima kuwepo na ushirikiano  baina ya wafanyakazi na mwajiri ikiwemo pia ushirikishwaji katika kutoa maamuzi  kwenye masuala mbalimbali ya chuo.


Kaimu Katibu wa Chama cha Wafanyakazi RAAWU tawi la SUA Farida Mkongwe Kurunge akisoma risala ya wafanyakazi mbele ya Mgeni Rasmi

“Unaposhirikishwa katika kutoa maamuzi inapelekea  utekelezaji wa majukumu kuwa mwepesi kwani unakuwa unatekeleza maamuzi yako, wafanyakazi wanapotimiza wajibu wao ipasavyo  wanakuwa na matumaini ya  kupata stahiki zao  kwa wakati  hivyo tunashauri na  kuhimiza  kila mfanyakazi atimize wajibu wake kwa mwajiri” Amesema Farida Mkongwe  

Maadhimisho ya siku ya wafanyakazi mwaka huu yamepambwa na kaulimbiu isemayo  ‘Mishahara  na maslahi bora  kwa wafanyakazi  ndio kilio chetu kazi iendelee’ ambapo jumla ya wafanyakazi hodari 6 na wafanyakazi 

Post a Comment

0 Comments