Gerald
Lwomile
Afisa wa TAKUKURU mkoani Arusha Bi. Jacqueline Kapile aliyesimama akiongea na watumishi wa SUA Kampasi ya Olmotonyi
Pongezi hizo zimetolewa na Afisa wa TAKUKURU mkoani
Arusha Bi. Jacqueline Kapile Februari 23, 2022 wakati akitoa mafunzo ya maadili ambayo ni nguzo muhimu
katika mapambano dhidi ya rushwa kwa Wafanyakazi wa Chuo Kikuu cha Sokoine
cha Kilimo Kampasi ya Olmotonyi
Akizungumza katika mafunzo hayo Bi. Kapile amesema
pamoja na SUA kutoa fursa hiyo lakini ni muhimu kwa watumishi hao kujenga jamii
yenye uadilifu kwa kuhakikisha wanajenga maadili toka nyumbani kwani mzazi anao
wajibu mkubwa wa kujenga maadili ya mtoto lakini pia na yeye kuwa na maadili
mema
“Kama wazazi tunao wajibu mkubwa kuhakikisha
tunawajenga watoto wetu katika misingi ya maadili, unakuta mtoto ili atumwe
anauliza utanipa shilingi ngapi hapana haya si maadili kwa hiyo tuwakumbushe
Watoto kuwa nimekutuma kama mzazi”amesema Kipile
Aidha
Bi. Kapile amesema watumishi wa Serikali au Umma wanapotamani kuishi maisha ya
anasa ambayo hayalingani na kipato chao halisi, huwa mwanzo wa kujihusisha na
rushwa.
“Mtumishi
huyu huanza kubuni mbinu itakayompatia fedha kwa haraka, matokeo yake huangukia
katika vishawishi vya kupindisha haki na maadili ilimradi kaahidiwa au kupewa hongo” amesema Bi. Kapile
Akizungumza katika kikao hicho Meneja wa Kampasi ya Olmotonyi Bw. Said Sallum Kiparu amesema katika kuhakikisha kunakuwa na uwajibikaji ni muhimu kuhakikisha kila mtumishi anafanya kazi kwa bidii na kuleta ufanisi katika eneo la kazi
Meneja wa Kampasi ya Olmotonyi Said Sallum Kiparu aliyekaa katikakati akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na wajumbe wa KKU na watumishi wa SUA Kampasi ya Olmotonyi
Amesema jambo la uaminifu katika kazi ni jambo la
msingi na linaweza kusaidia kuondoa mgongano wa kimaslahi kwa mtumishi na
kusababisha kuwepo kwa maendeleo makubwa katika jamii
Akitoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali Mwenyekiti wa
Kamati ya Kudhibiti Uadilifu SUA Prof. Christopher Mahonge amesema wafanyakazi
wanao wajibu mkubwa wa kuhakikisha wanachangia katika maendeleo ya taifa kwa
kufanya kazi kwa bidii
Amesema kamati yake imefungua milango kwa kila mtumishi
katika taasisi hiyo kutoa taarifa za ukiukwaji wa maadili na kuwa mtoa taarifa
atalindwa kutokana na sheria, kanuni na miongozo ya utoaji taarifa.
0 Comments