Na Farida
Mkongwe
Katibu
Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Maganga
amezindua rasmi Mradi wa Kujenga Uwezo wa Taasisi ili Kupunguza Hewa Ukaa
inayosababishwa na ukataji miti na uharibifu wa misitu unaojulikana kwa jina la
REDD+
Mkurugenzi wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Andrew Komba akizungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi kufanya uzinduzi wa Mradi wa REDD+ |
Akizindua
Mradi huo ambao unafadhiliwa na Serikali ya Norway Bi. Mary amesema kimsingi
mradi wa REDD+ utasaidia kuharakisha zoezi la kuhifadhi misitu kwa njia
mbalimbali ikiwemo upandaji wa miti na kuhifadhi vyanzo vya maji.
“Kwa
hiyo Mradi huu ambao tumeuzindua utatusaidia kuwa na Mikakati endelevu ya
kutunza na kuhifadhi misitu, tuelewe mabadiliko ya tabianchi yanaathiri dunia
nzima lakini kwa sisi bado tunaweza kuirudisha ardhi kama ilivyokuwa kwa
kupanda miti na kutunza vyanzo vya maji ili kusaidia na kwingine ambako
kumeshaharibika”, amesema Katibu huyo.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Andrew
Komba amesema Mradi wa REDD+ utasaidia sana kwani kwa sasa takribani wastani wa
hekta 469,000 zinakatwa kwenye misitu hapa nchini kwa ajili ya matumizi
mbalimbali
“Kasi
hii ya ukataji miti sio nzuri kwa maendeleo au mustakabali wa mazingira yetu,
sasa tunakwenda kutafuta nishati mbadala, tunataka kutumia kilimo ambacho
hakitumii maji mengi, tutahakikisha wafugaji wanapata malisho na maji kwenye
maeneo yaliyoendelezwa badala ya kutumia vyanzo vya maji”, amesisitiza Dkt.
Komba
Naye
Mratibu wa Program wa Shirika la Mazingira IUCN Kanda ya Afrika Mashariki na
Kusini Charles Oluchina amewaomba watanzania kutoa ushirikiano kwa sababu
Tanzania ni nchi muhimu sana kwenye kilimo.
“Mchango
wa kilimo kwa Tanzania, Afrika mashariki na Kusini ni mkubwa sana, mazao
yanayotokea Tanzania yanalisha hadi Angola, Kusini Sudan hadi sehemu za Kenya”,
amesema Mratibu huyo.
Mradi
wa REDD+ awamu ya pili umezinduliwa Februari 23, 2022 ukiwa na lengo la
kuiwezesha Tanzania kuwa tayari katika utekelezaji wa Makubaliano ya Paris
kuhusu mabadiliko ya tabianchi (Paris Agreement) ili kunufaika na
biashara ya hewa ukaa ifikapo 2022.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Maganga akitoa hotuba ya uzinduzi wa Mradi REDD+ mjini Morogoro |
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Maganga (wa nne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wengine waliohudhuria kwenye uzinduzi huo |
0 Comments