SUAMEDIA

Rwanda kutositisha kutoa chanjo ya AstraZeneca

RWANDA 

Serikali Rwanda imesema haitasitisha mpango wa kutoa chanjo ya AstraZeneca.



Afisa mkuu Wa mamlaka ya afya Dkt Sabin Nsabimana amewaambia waandishi wa habari mjini Kigali kwamba chanjo ya Astrazeneca haina madhara.

Tangu wiki mbili zilizopita Rwanda imeishatoa chanjo kwa watu wapatao laki mbili na hamsini na saba elfu (257,000 ) ambapo zaidi ya theluthi mbili walipewa chanjo ya AstraZeneca na wengine chanjo ya Pfizer.

Rwanda inatarajia kupata dozi za chanjo ya corona milioni moja na tisini na nane elfu miatisa sitini (1,098,960,) aina ya AstraZeneca/Oxford na Pfizer-BioNTech, zitatolewa kwa awamu wa kwanza na wa pili wa mwaka 2021.


Post a Comment

0 Comments