Na.Vedasto George.
Wakulima na wafugaji nchini
wameshauliwa kutumia mbinu bora za kilimo zinzoweza kutunza mazingira ili kizazi cha sasa na kijacho kiweze kunufaika
na kilimo kwa manufaa ya jamii na taifa kwa ujumla.
Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Uzamili, Utafiti, Uhaulishaji wa Teknolojia na Ushauri wa Kitalaamu Prof. Erson Karimuribo aliyekaa katikati akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa warsha kulia waliokaa ni Mkurugenzi wa ICE Prof. Mwaseba na kushoto ni Prof. Sibuga
Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Kurugenzi
ya Uzamili, Utafiti, Uhaulishaji wa Teknolojia na Ushauri wa Kitalaamu Prof.
Erson Karimuribo kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA wakati
akifungua warsha wa siku mbili ulio wakutanisha wadau mbalimbali wa kilimo, wanafunzi wa SUA, Wataalamu kutoka
mashirika ya kiserikali na yasiyo ya kiserikali ya ikolojia pamoja na wanafunzi kutoka chuo cha Nelsoni
Mandela kwa ajili ya kuchangia na
kubadilishana uelewa wa namna ya kuendeleza kilimo ikolojia Tanzania.
“Kilimo Ikolojia imekuwa ni dhana mpya kwa
ajiri ya kuendeleza kilimo kwa sababu ya
mazingira siku za zamani kilimo chetu kilikuwa kinafuata taratibu bila ya
kujali mazingira lakini sasa ivi tumeunganisha hizi tasinia mbili kilimo halisi
pamoja na dhana nzima ya ikolojia ambayo inajali mazingira”Amesema Prof. Karimuribo
Aidha Prof. Karimuribo amesema kutokana na changamoto ya
uaribifu wa mazingira uliopo nchini kwa sasa
kilimo ikolojia kitasaidia kutunza mazingira Zaidi ya miaka 50 ijayo na
kupunguza athari kwa wananchi.
“Tumeanza na mikoa ambayo inatuzunguka
pamoja na wilaya zetu za mkoa wa Morogoro ambazo ni Mvomero pamoja na wilaya ya
Morogoro mjini kwa sababu tunaona ni muhimu, pia tuna mkoa wa Mbeya,Arusha”
Amesema Prof. Karimuribo
Kwaupande
wake Mratibu wa Mradi wa Kilimo Ikolojia
Tanzania SUA, ambaye pia ni Mhadhili Mwandamizi kutoka Chuo kikuu cha Sokoine
cha Kilimo SUA amesema lengo la mradi huo ni kufanya mageuzi katika kilimo,
kuboresha Maisha ya mtanzania na
kuifadhi mazingiara
Kupitia
huu mradi tunategemea kuongeza
rasilimali watu kwa maana ya kupitia
mafunzo shahada ya juu ya uzamivu na uzamili na pia inatoa fursa kwa wanafunzi
wa shahada ya kwanza kufanya utafiti chini ya mradi lakini mwisho wa siku tukipata tafiti hizo
tuweze kuzisambaza kwa wakulima”Alisema Prof Mwaseba .
Naye
Prof. Kalunde Sibuga kutoka Idara ya
Mimea Vipando na kilimo cha Busitani na kiongozi katika Mradi wa uimarishaji wa
Vyuo Vikuu unaoshirikiana na Mradi wa
Kilimo Ikolojia amesema lengo la mashirikiao hayo ni kujenga kuwajengea uwezo
wataalamu watakaofanya utafiti na kutengeneza Teknolojia zitakazotumiwa
mashambani.
Mradi wa Kilimo Ikolojia Tanzania Katika Chuo Kikuu
Cha Sokoine Cha kilimo SUA unafadhiliwa na mradi wa Mc Knigth wenye makao yake
makuu nchini Marekani
0 Comments