SUAMEDIA

Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA chatoa mafunzo kwa Wasindikaji wa vyakula

Na Ayoub Mwigune

 Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA  kimeandaa Semina kwa ajili ya mafunzo kwa Wasindikaji wa vyakula mbalimbali kutoka manispaa ya Morogoro yenye lengo la kuhakikisha kazi mbalimbali za kitafiti na kiteknolija  za Chuo hicho zinawafikia Watu mbalimbali katika Jamii.




Washiriki wa mafunzo wakifuatilia mafunzo kutoka kwa mwezeshaji hayupo pichani 

Akifungua Semina hiyo Chuoni hapo Prof. Esron Karimuribo  ambaye ni Mkurugenzi wa Kurugenzi ,Uzamili, Utafiti, Uhaulishaji wa Teknolojia na Ushauri wa Kitaalam kutoka SUA   amesema  lengo la semina hiyo ni kuhakikisha kuwa kazi za Kitafiti zinazofanywa na Chuo hicho zinawafikia Wakulima

Prof. Karimuribo  amesema malengo mengine ya Semina hiyo ni kuwaunganisha Wakulima pamoja na Wataalamu  na huduma zinazopatikana katika chuo hicho ili kuweza kuwasaidia wasindikaji hao kuweza kuhakiki ubora na kuwasaidia kuweza kupata ithibati kutoka shirika la viwango nchini TBS na  kuongeza  kipato chao

Naye  Dk. Doreen Ndossi ambaye ni Mratibu wa Mhaulishaji wa Teknolojia kutoka SUA amesema Chuo hicho kimeanzisha kitengo  cha Teknolojia kinachofahamika kwa jina SUA Innovatiation Hub ambacho kina lengo la kuhakikisha kila Teknolijia na Ubunifu unawafika Walengwa  katika Jamii

Kwa upande wake Dkt. Beatrice Kilima ambaye ni mhadhiri, Idara ya Teknolojia ya Chakula, Llishe  na Sayansi ya Mlaji na Muwezeshaji katika Semina hiyo amesema mafunzo hayo yanawajengea uwezo Wajasiriamali katika Kuzalisha Vyakula  ambavyo vitakuwa na ubora na usalama kwa ajili ya afya ya Walaji pamoja kanuni bora za usafirishaji wa Chakula na jinsi ya kuweza kupata nembo ya ubora kutoka TBS


Washiriki wa mafunzo wakiwa katika mjadala

Bw.Ibrahim  Diwani pamoja na Monica Yohana kwa pamoja wamesema Mafunzo  hayo yamewafunza  namna ya kuzingatia usafi wakati wa uzalishaji ,namna ya kuzalisha Bidhaa bora pamoja na kuweza kuingia katika ushindani wa soko .


Post a Comment

0 Comments