SUAMEDIA

Maafisa Mawasiliano nchini watakiwa kutafuta maarifa

 

Calvin Gwabara

Dar es Salaam

Wataalamu wa masuala ya Menejimenti ya Maarifa na Maafisa Mawasiliano nchini  wametakiwa kuamka kutafuta maarifa hayo kutoka kwenye maeneo mbalimbali yanakozalishwa na kuyafikisha kwa jamii ili yakajibu changamoto zinazoikabili jamii katika kukuza uchumi wao na Taifa.

Mshauri namwezeshaji wa kimataifa Bwana Martin Muchero akileza na kufafanua maana ya Maazimio ya Malabo na yanavyotekelezwa kila nchi Mwananchama.

Wito huo umetolewa na Meneja wa Mawasiliano na Menejimenti ya Maarifa kutoka Taasisi ya Utafiti Tanzania (TARI) Dkt. Richard Kasuga wakati akiwasilisha mada yake kuhusu Menejimenti ya Maarifa nchini hasa katika sekta ya kilimo kwa maafisa menejimenti ya maarifa na mawasiliano kutoka katika taasisi mbalimbali za utafiti, vyuo vikuu na maeneo mengine.

“Maarifa yapo mengi sana kwenye vituo vyetu vya utafiti,vyuo vikuu na maeneo mengine yanayozalisha maarifa lakini jamii yetu hasa wakulima hawawezi kufika kuzifuata na kuzitafuta huko lakini sisi kama wataalamu wa menejimenti ya maarifa tunaweza kwenda kuzichimbua na kuwaletea wananchi wetu kuzitumia na kubadilisha maisha yao. Alisema Dkt. Kasuga.

Dkt. Kasuga amesema kwenye kurasa za taasisi mbalimbali ikiwemo Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo kupitia Mkulima Library, Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania TARI, TARIRI, Mamlaka ya Hali ya Hewa, NIMRI na nyingine nyingi kumewekwa maarifa mbalimbali wanayozalisha ambayo yanahitajika na wakulima na wafugaji hivyo ni jukumu la wataalamu hao wa mawasiliano na menejimenti ya maarifa kuzitembelea na kuchukua yanayohitajika ili jamii ikayatumie.

Meneja huyo wa menejimenti ya maarifa na mawasiliano wa TARI ameongeza kuwa siku hizi zipo njia nyingi za kufikisha maarifa kwa jamii ambazo jamii inazitumie ikiwemo mitandao ya kijamii,kama vile twitter, facebook, Instagram lakini pia Televisheni, Redio na Magazeti ambazo wanaweza kuzitumia kufikisha  elimu kwa walengwa kirahisi.

Tanzania inaendesha mafunzo  ya kitaifa ya siku nne ya kuwajengea uwezo Maafisa Mawasiliano, Wagani na Waandishi wa Habari namna ya kuchakata matokeo ya Tafiti na kuwafikishia walengwa sambamba na kufuatilia na kutoa taarifa za utekelezaji wa maazimio ya Malabo ulioandaliwa na Taasisi ya Uratibu wa Tafiti za Kilimo (CCARDESA) kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI).

 


Bwana Shadrack Ndalawa msimamizi wa dawati la CAADP Wizara ya Kilimo akieleza utekeeleaji wa maazimio Malabo upande wa Tanzania.




Afisa Habari na Menejiment ya Maarifa kutoka kutoka Taasisi ya Uratibu wa Tafiti za Kilimo Afrika (CCARDESA) Bi. Bridget Kakulwa akieleza akieleza matarajio ya Mafunzo hayo.

Meneja wa Mawasiliano na menejimenti ya Maarifa kutoka Taasisi ya Utafiti Tanzania (TARI) Dkt. Richard Kasuga akieleza malengo ya Mafunzo hayo ya Kiataifa ya siku nne kwa Maafisa mawasiliano, Wanahabari na wadau wengine.


Afisa Programu ya CAADP -XP4, Bi. Futh Magagula akitoa salamu za Taasisi ya Uratibu wa Tafiti za Kilimo Afrika (CCARDESA) wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo jijini Dar es salaam.


Meneja wa Kituo cha Utafiti cha TARI Mikocheni Dkt.Joseph Ndunguru akifungua mafunzo hayo ya kitaifa ya siku nne kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TARI.

Post a Comment

0 Comments