Na: Asifiwe Mbembela
Chuo Kikuu cha Sokoine cha
Kikili (SUA) kinatarajia kuandika historia mpya kufuatia kufanyika kwa Hafla ya
Uwekaji wa Jiwe la Msingi kwa ajili ya ujenzi wa Jengo la Taaluma na Bweni
katika Kampasi ya Mizengo Pinda, itakayofanyika siku ya Jumamosi, tarehe 14
Machi, 2026.
Mgeni Rasmi, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye anatarajiwa kuweka jiwe la msingi kuashiria mwanzo wa utekelezaji wa mradi huo muhimu wa kimkakati.
Ujenzi wa majengo hayo
unatekelezwa kwa ufadhili wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi
(HEET), unaolenga kuimarisha miundombinu ya kufundishia na kujifunzia vyuo
vikuu nchini.
Mradi huu pia utaboresha mazingira ya malazi kwa wanafunzi na hivyo kuongeza ufanisi wa shughuli za kitaaluma pamoja na ustawi wa wanachuo kwa ujumla.
Kupitia mradi huu, Chuo
kitaongeza uwezo wa kuhudumia wanafunzi wengi zaidi sambamba na kuboresha ubora
wa mazingira ya kujifunzia, jambo litakalochochea maendeleo ya taaluma, tafiti
na ubunifu.
Maboresho haya ni sehemu ya
mkakati mpana wa Serikali wa kuimarisha sekta ya elimu ya juu ili kuzalisha
wataalamu wenye ujuzi na ushindani katika soko la ajira.
Chuo kinatoa pongezi za dhati
kwa Serikali kwa kuendelea kuwekeza katika maendeleo ya elimu ya juu na
miundombinu yake, uwekezaji huu unaonesha dhamira thabiti ya Serikali ya
kuhakikisha vyuo vikuu vinakuwa na mazingira bora yanayowezesha utoaji wa elimu
yenye ubora wa kimataifa.


.jpg.jpeg)
0 Comments