Na: Farida Mkongwe
Chuo
Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimefanikiwa kupata miradi mipya ya utafiti
36 yenye thamani ya Shilingi bilioni 10.5, inayolenga kufanya tafiti
zinazoongeza maarifa na kutatua changamoto katika sekta za kilimo, mifugo,
mazingira na maendeleo ya jamii.
“Tangu
Mahafali ya 45 yaliyofanyika Mei 22, 2025, Baraza limefanikisha utekelezaji wa
shughuli mbalimbali zilizolenga kuboresha utendaji wa Chuo katika maeneo
tofauti, likiwa na lengo kuu la kuhakikisha SUA inaendelea kuwa taasisi mahiri
ya elimu ya juu, utafiti na utoaji wa huduma bora kwa jamii,” amesema Mhe.
Massawe.
Aidha, amesema pamoja na mafanikio hayo, Baraza la Chuo linaendelea kuimarisha vyanzo mbadala vya mapato kupitia miradi ya kibiashara, utoaji wa ushauri wa kitaaluma na uwekezaji katika maeneo ya kimkakati, sambamba na kuhimiza matumizi ya matokeo ya tafiti katika sera na mipango ya maendeleo ya taifa.
0 Comments