Na Josephine Mallango
Mkurugenzi wa Ithibati kutoka Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) Dkt. Telemu Kassile amekipongeza Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kwa kuendana na kasi ya mabadiliko ya Sera mpya ya Elimu ya 2023 inayosisitiza mitaala ya sasa ambayo itawapa wahitimu ujuzi wa kuweza kuajiriwa au kujiari popote watakapokuwa mara baada ya kuhitimu masomo yao.
Akifungua warsha Mkoani Morogoro Dkt. Kassile amesema SUA wameandaa mafunzo ya siku 5 ya kuwajengea uwezo wanataaluma na viongozi mbalimbali katika ngazi tofauti tofauti SUA mara baada ya kuhuisha mitaala yake, na kutengeneza mitaala mipya iliyozingatia hali halisi.
"Pongezi SUA, wanaenda na kasi ya mabadiliko Mafunzo haya yanalenga zaidi katika kuwapa mbinu washiriki ya namna ya kufundisha mitaala iliyofanyiwa marejeo baada ya sera ya elimu na mafunzo ya mwaka 2014 kufanyiwa mapitio na kutolewa toleo la mwaka 2023 kwa kuwa sera hiyo imesisitiza zaidi wahitimu kuweza kuwa na na ujuzi na sisi TCU kama wasimamizi tulitoa maelekezo kwa vyuo vikuu vyote nchini kuhuisha mitaala yao na wanaoandaa mitaala mipya waweze kuandaa mitaala ambayo itawapa wahitimu ujuzi wa kuweza kuajiriwa au kujiari” amesema Kassile.
Ameongeza kuwa Sehemu kubwa ya mafunzo kwa sasa mwanafunzi ataweza kujifunza wenyewe na kushirikiana na wenzake tofauti na mfumo wa zamani ambao mwalimu alisimama mbele na kufundisha kile anachojua sanjari na mabadiliko katika mfumo wa mafunzo kwa vitendo ambapo kwa sasa mwanafunzi mwaka wa mwisho atakaa sehemu ya mafunzo ya vitendo kwa semista nzima ili ajifunze stadi za kazi na mazingira ya kazi ili akimaliza anakuwa tayari kuanza kazi tofauti na mfumo wa zamani mwanafunzi alikuwa anaenda mafunzo kwa vitendo kwa wiki 5.
Nae Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Mipango , Utawala na fedha Prof. Amandus Muhairwa amesema katika mafunzo haya wanawataka wataalamu wote wa SUA wafanye wanachoongea kwa vitendo ili nwanafunzi aone uhalisia wake akijua hiyo ndio ajira yake na vile vile wataalamu hao kuwasukuma wanafunzi katika kutenda zaidi uhalisia wa kupata matokeo.
Warsha
hiyo imeandaliwa na Mradi wa TAGDev 2.0 AGRIFOSE–RIH ni sehemu ya Programu ya
RUFORUM kwa ushirikiano kati ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA),
Chuo cha Nelson Mandela (Arusha), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), na
Jukwaa la Vyuo Vikuu Afrika (RUFORUM) kwa ufadhili wa Mastercard Foundation ni
mradi wa miaka 5.
0 Comments