Na: Gerald Lwomile
Serikali
imesema pamoja na kuongezeka kwa uzalishaji wa zao la Kahawa kutoka tani 55
elfu hadi kufikia tani 85 elfu katika kipindi cha miaka 3 inafanya maboresho
makubwa ya sera zake za kilimo kwani zimekuwa kikwazo katika kuleta maendeleo
ya kilimo nchini.
![]() |
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu ka Serikali Gerson Msigwa akizungumza na waandishi wa habari |
Hayo
yamesemwa tarehe 16 februari, 2025 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa
na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa wakati akitoa taarifa
kuhusu masuala mbalimbali yaliyotekelezwa na serikali wakati wa mkutano na waandishi wa habari katika Bwawa la kufua
umeme la Julius Nyerere Rufuji mkoani Pwani.
Akizungumzia uzalishaji wa zao la Kahawa
nchini Msemaji Mkuu wa Serikali amekiri kuwa sera mbalimbali za Serikali kwa
wakati fulani zimekuwa si rafiki na kupelekea changamoto katika kilimo na soko
la Kahawa nchini.
Msigwa amesema hivi sasa
takwimu zinaonesha kuwa kuna nchi 50
zinazozalisha kahawa duniani ambapo kati ya hizo bara la Afrika ni 25 na kuwa nchini Tanzania uzalishaji wa
kahawa katika kipindi cha miaka 3 umeongezeka kutoka tani 55 elfu hadi tani 85
elfu.
Amesema tarehe 21 na 22 Februari,
2025 Tanzania itakua mwenyeji wa mkutano wa tatu wa Afrika wa Kahawa G25,
utakaofanyika katika ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es
Salaam.
Tarehe 1 Juni, 2022 Mkuu wa Mradi
wa utafiti wa 'TRADE HUB' Prof. Ruben Kadigi akitoa matiokeo ya awali ya utafiti
juu ya kutambua faida za kiuchumi, kijamii na kimazingira zinazotokana na
biashara ya Kahawa nchini alitaja changamoto kadhaa ikiwa ni pamoja na sera
pamoja na bei ya Kahawa kutokuwa rafiki katika uwekezaji wa zao hilo.
Akizungumzia suala la Umeme
msemaji wa Serikali amesema watanzania wawe na subira juu ya gharama za umeme
kwani kuwa juu kwani inaangalia namna
bora zaidi ya kuhakikisha umeme unakuwa
na gharama nafuu tofauti na sasa.
Amesema nchi imefanya uwekezaji
mkubwa katika uzalishaji wa umeme kwani mbali na kuwa na Bwawa la kuzalisha
umeme la Julius Nyerere Rufiji mkoani Pwani ina miradi kadhaa mingine mingi
ikiwa ni pamoja na mradi wa Rusumo utakaozalisha Megawati 80, Mradi wa
Kuzalisha Umeme kwa Kutumia Gesi Asilia wa Kinyerezi ‘I Extension’
utakaozalisha Megawati 185.
Ametaja Miradi mingine ni Mradi
wa Kuzalisha Umeme kwa Kutumia Maji wa Malagarasi Megawati 49.5 Mradi wa
Kuzalisha Umeme kwa Kutumia Maji wa Kakono Megawati 87 na Mradi wa umeme wa jua
ulianzishwa katika Wilaya ya Kishapu Mkoani wa Shinyanga wenye uwezo wa
kuzalisha jumla ya Megawati 150.
Kusikiliza zaidi bofya 👇
0 Comments