Na: Siwema
Malibiche
Wafanyakazi nchini wametakiwa kujiunga na vyama vya
wafanyakazi ikiwemo RAAWU ili kusaidia kuwa na sauti ya pamoja mahala pa kazi
itakatowezesha kuboresha namna ya utekelezaji wa majukumu yao kwa kufuata haki
na wajibu.
Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa RAAWU Tawi la SUA Bw. Faraja
Kamendu baada ya kumalizika kwa Semina ya wafanyakazi wa SUA na Wanachama wa RAAWU Tawi la SUA iliyofanyika
Kampasi ya Edward Moringe mjini Morogoro ambapo amewasisitiza wafanyakazi kuona
umuhimu wa kujiunga na vyama vya wafanyakazi kwa maslahi yao binafsi na kwa taifa.
Amesema RAAWU imemua
kufanya semina hiyo baada ya kufanya tafiti mbalimbali na kugundua kuwa wafanyakazi wengi hawana
elimu ya kustaafu na namna ya kuwekeza wanapokuwa kazini na kuamua kuja na
mafunzo kwa wastaafu watarajiwa kwa kuwajengea uwezo utakaosaidia kuyaelewa mazingira yao baada ya kustaafu kwa
kuwekeza ili kuepuka changamoto
Kwa upande wake, Katibu wa RAAWU Mkoa wa Morogoro Bi. Agness Gwau amesema uongozi wa chama hicho umeamua kutoa mafunzo hayo ili kuwajengea misingi bora ya kiuwekezaji kwa wafanyakazi na kuongeza kuwa kama uongozi utaendelea kuyaleta mafunzo mara kwa mara ili kuwajenga kiutendaji wanachama wake
Naye Mmoja wa
washiriki katika Semina hiyo Bw. Haroun Kapingo ambaye ni Mtumishi kutoka SUA amesema semina
hiyo imekuwa ni ya manufaa zaidi kupitia
mafunzo waliyopewa kwani imewapatia uelewa wa haki na wajibu wao kama
wafanyakazi na namna nzuri ya kujiandaa katika
uwekezaji kabla ya kustaafu.
Aidha ameupongeza uongozi wa RAAWU SUA kwa kuyaleta mafunzo hayo ya siku mbili kwa wafanyakazi ambayo anaamini yataleta tija huku akiwasisitiza washiriki wote wa mafunzo hayo kutekeleza kwa vitendo yale yote waliyojifunza ili kuepuka changamoto zinazoweza kujitokeza wakiwa kazini na baada ya kustaafu.
Semina hiyo ya siku mbili kwa wanachama wa RAAWU na
wafanyakazi wa SUA ambayo imeandaliwa na chama cha RAAWU Makao Makuu kwa
kushirikiana na RAAWU Tawi la SUA imewawezesha washiriki kujifunza elimu ya
vyama vya wafanyakazi, njia za kusaidia katika ukuaji wa taaluma kazini na
maandalizi ya kustaafu.
Kauli mbiu ya chama hicho ni “Elimu kwanza, Nguvu ya hoja,
Kwa maslahi bora ya Wafanyakazi.
0 Comments