SUAMEDIA

Biashara ya Kaboni ni Ukombozi kwa Taifa

 

Na: Mwandishi wetu

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Masauni amesema Kituo cha Taifa cha Ufuatiliaji  wa Kaboni (NCMC) nchini kilichopo Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kitakuwa  ni miongoni mwa Taasisi muhimu katika kusaidia Taifa kutokana na  miradi mbalimbali ambayo  mataifa ya nje yanakuja kuwekeza kupitia biashara ya Kaboni, ili biashara hiyo iweze kusaidia katika kukuza kipato cha wananchi lakini pia kuchangia uchumi wa nchi kwa ujumla.




Mhandisi Masauni ameyasema hayo Februari 10, 2025 wakati alipofanya ziara ya kutembelea Kituo hicho kilichopo mkoani Morogoro.

Mapema Mkuu wa Wilaya ya Kilosa  Shaka Hamdu Shaka ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro katika ziara hiyo  amesema mkoa huo umejipanga kutumia vyema fursa hiyo ili kutekeleza na kutafsiri kwa vitendo maelekezo na maono ya Rais Samia ya kuhakikisha  biashara ya Kaboni inakuwa vyanzo vingine vya kuinua kipato cha wananchi na kuchangia katika maendeleo nchini.


"Ni fursa muhimu sana kwetu uwepo wa kituo hiki mkoani kwetu ni hatua muhimu sana, kwani vianzio vyote vinavyopelekea biashara hii kufanyika tunavyo kupitia misitu, mifugo na mito tutahakikisha fursa hii inatumika vyema na tija iweze kuonekana kwa wananchi na Taifa kwa ujumla kupitia rasilimali tulizonazo" , alisema Shaka.






Post a Comment

0 Comments