Na: Ayoub Mwigune
Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA)
kimewapeleka Askari wasaidizi (Auxiliary
Police) 10 kutoka Idara ya Usalama chuoni hapo kwenye Mafunzo maalum kwa muda
wa miezi mitatu katika Chuo cha Kidatu mkoani Morogoro kwa lengo la kuongezea
ufanisi kwenye kazi zao.
Hayo yamebainishwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi Saimoni Haule ambaye pia ni Mshauri Mkuu na Msimamizi wa Askari wasaidizi wa kituo cha Usalama SUA wakati akizungumza na SUAMEDIA kwenye tukio la kuwaaga Askari hao.
Amesema kuwa hiyo ni nafasi adimu na ya
kipekee hivyo anategemea kuwa Askari hao watazingatia kwa umakini Mafunzo hayo
na watakaporejea katika majukumu yao weledi utaongezeka hasa katika kazi yao ya
msingi ya kusimamia ulinzi na usalama wa
Chuo na kuhakikisha wanafunzi pamoja na wafanyakazi wanafurahia matunda ya
mafunzo hayo kwa kuwa salama.
“Masuala ya ulinzi jamii yanaenda kuimarika
hasa kwa upande wa jinsia , ulinzi wa watoto, wanawake lakini pia makundi
maalum, zaidi ni kwenda kuboresha kazi zetu za kila siku hivyo mwisho wa siku nidhamu
inahitajika ili kuhakikisha wanakwenda kufuzu mafunzo hayo kwa niaba ya jumuiya
ya SUA”, amesema Kamishna huyo Msaidizi wa Polisi .
Kamishna Msaidizi wa Polisi Haule ameishukuru
Menejimenti ya SUA, Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini
(IGP) Camillus Wambura kupitia Kamisheni
za Jeshi la Polisi ikiwemo ya Operesheni na Mafunzo pamoja na Polisi jamii kule ambako wanasimamia Makampuni ya
ulinzi binafsi kwa kuwapatia nafasi ya kwenda kuongeza ujuzi katika kazi lengo
likiwa kuimarisha ulinzi na usalama.
Kwa upande wake Arod Ngalya na Sabina Sumwa ambao ni miongoni mwa Askari
Wasaidizi SUA wanaokwenda kwenye mafunzo
hayo wamesema wanaishukuru Menejimenti ya Chuo hicho kwa kuwapatia nafasi hiyo
na kuahidi kuyatumia mafunzo hayo kuwa watendaji
kazi wazuri na kuwafundisha wenzao kile watakachojifunza wakiwa Chuo cha Kidatu.
0 Comments