SUAMEDIA

Woga wa kisichojulikana unawagharimu Wakulima Barani Afrika.

 Na: Calvin Edward Gwabara - Nairobi

Woga usiojulikana unsababisha Viwavijeshi vamizi kushambulia zaidi ya tani milioni 20 za Mahindi ya wkakulima ambayo yengeweza kulisha zaidi ya watu milioni 100.

Meneja wa Mradi wa Mahindi wa TELA Dkt. Sylvester Oikeh wakati akiwasilisha mada.

Hayo yamebainishwa na Meneja wa mradi wa Mahindi wa TELA Dr. Sylvester Oikeh wakati akiwasilisha mada kuhusu uwezeshwaji wa uhimilivu wa changamoto za kilimo kupitia Sayansi Teknolojia na Ubunifu wakati kwenye Mkutano wa Teknolojia za Kilimo Barani Afrika unaoendelea Jijini Nairobo Nchini Kenya.

“ Pamoja na Mamlaka mbalimbali duniani za uthibiti ubora kuthibitisha kuwa mazao yatokanayo na Tenkolojia ya Uhandisi jeni ( GE) kuwa ni salama kwa binadamu na mazingira lakini bado teknolojia hiyo inazuiliwa na baadhi ya watu kwa kuwatisha wananchi hasa wakulima kuhusu usalama wake” Alieleza Dkt.  Sylvester.

Aliongeza “Kuna nchi hadi sasa hazitumii teknolojia hiyo ingawa tafiti zimekamilika kwa sababu moja tuu ya kutokuwa na sheria ambayo inaruhusu au kuwa rafiki kwenye hatua ya ubiasharishaji wa mazao ya bioteknolojia yaani GMO”.

Amesema kuwa zao la mahindi ndilo linaloshambuliwa zaidi na kiwavijeshi vamizi kutoka amerika na ni zao ambalo linategemewa kwa chakula na na zaidi ya watu milioni 300 barani afrika hivyo jitihada za makusudi zinahitajika katika kutumia teknolojia kuwakabili wadudu hawa ambao wanasabaisha njaa na umasikini kwa wakulima.


                 PICHA WASHIRIKI WAKIFUATILIA WASILIHO.










Post a Comment

0 Comments