SUAMEDIA

Watumishi SUA ni muhimu kuwa na roho ya kusikilizana na kujifunza - Prof. Mahonge

 

Na Gerald Lwomile - Arusha

Mwenyekiti wa Kamati ya Kuthibiti Uadilifu Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) Prof. Christpher Mahonge amesema ni muhimu wafanyakazi wawe na roho ya kusikiliza ili kujifunza zaidi na kuwa na maelewa katika maeneo ya kazi ili kuleta tija.


Prof. Mahonge amesema hayo leo Septemba 29, 2023 wakati akizungumza na wafanyakazi wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo,  Kampasi ya Olmotonyi mkoani Arusha.

Amesema ni muhimu watu kujua namna njema na sahihi ya kuishi pamoja na kuchukuliana ili kuleta tija katika kazi kwani ili taasisi iweze kutimiza malengo yake ni lazima kuwa na hali ya kutegemeana miongoni mwa watumishi.


Mwenyekiti wa KKU, Prof. Mahonge kushoto akiwasili katika ukumbi wa mikutano Kampasi ya Olmotonyi, kulia ni Meneja wa Kampasi ya Olmotonyi Bw. Kiparu na katikati ni Prof. Katakweba ambaye ni mjumbe wa KKU SUA (Picha na Gerald Lwomile)






Meneja wa Kampasi ya Olmotonyi Bw. Said Kiparu akizungumza kabla ya kuanza mafunzo



Mwenyekiti wa Kamati ya Kuthibiti Uadilifu SUA Prof. Mahonge akitoa mafunzo ya Uadilifu


Post a Comment

0 Comments