Na: Asifiwe Mbembela
Wanafunzi wa kidato cha tano na sita katika Shule ya Sekondari ya Dkt. Salmin Amour Juma iliyopo Chumbuni Mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar wametakiwa kuchangamkia fursa ya kusoma katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) ili kuweza kutimiza ndoto zao.
Bi. Mawesa Ukani, Afisa Udahili kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo akizungumza katika hadhara ya wanafunzi hao ambao ni mchanganyiko wa masomo ya CBG na PCB amesema kupitia masomo wanayosoma ufaulu unaohitajika ili wawe na sifa za kudahiliwa katika Chuo cha SUA ni ufaulu wa pointi 4 wa daraja DD au CE.
0 Comments