SUAMEDIA

Benki ya Dunia waridhika na utekelezaji wa miradi wanayoifadhili SUA

Na: Calvin Gwabara – Morogoro.

Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Nchini Tanzania Bw. Nathan Belete amepongeza Chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo kwa kutumia fedha zilizotolewa na Benki hiyo na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiano ili kuendeleza matokeo mazuri yaliyopatikana.

Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Nchini Tanzania Bw. Nathan Belete (wa  tatu kulia) akiapta maelezo kutoka kwa Prof. Appiah Massawe alipotembelea Kituo cha Umahiri cha mashariki na kusini mwa Afrika cha kudhibiti Panya na matumizi yake katika kunusa  (ACE IRPM & BTD). 

Hayo ameyasema wakati akizungumza na Uongozi na Watafiti wa Chuo hicho mara baada ya kupokea mawasilisho ya utekelezaji wa fedha zilizotolewa na Benki hiyo katika utekeelezaji wa miradi kwenye Taasisi ya afya moja inayoshughukikia magonjwa ambukizi kusini mwa jangwa la sahara (SACIDS), Mradi wa HEET na Kwenye kituo cha umahiri cha mashariki na kusini mwa Afrika cha kudhibiti panya na matumzi yake katika kunusa (ACE IRPM & BTD).

“Kwa kutambua mchango wa elimu kama mtaji wa binadamu ndio maana Benki ya Dunia tumeweka swala la elimu kama kipaumbele kwenye utekelezaji wa miradi yetu hivyo nitumie nafasi hii kuahidi Wizara ya Elimu pamoja na SUA kuwa tutaendelea kutoa ushirikiano katika kuteleza miradi kama hii ambayo inaleta tija kubwa kwenye maendeleo ya wananchi na Taifa” alisema Bwana Belete.

Bwana Belete amepongea kazi nzuri inayofanywa na SUA katika kutafuta ufumbuzi wa changamoto mbalimbali za taifa na kuahidi kushirikiana na Chuo hicho kwenye kusaidia ongezeko la udahili wa Wanafunzi kutokana na takwimu kuonesha udahili nchini Tanziania upo chini ikilinganishwa na nchi jirani.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Elimu ya Juu, Dkt Keneth Hosea akitoa salamu za Wizara ya Elimu ameiomba Benki ya Dunia kuona uwezekano wa kuongeza fedha kwenye miradi hiyo ili kazi nzuri iliyofanywa na miradi kwenye vituo hivyo vya umahiri iendelezwe zaidi.

“Kwakuwa kupitia mradi wa HEET unakwenda kuongeza nguvu kwenye kampasi 15 mpya kwenye vyuo mbalimbali vya umma nchini tunaomba Benki ya Dunia itusaidie kuongeza fedha kwenye eneo la Mafunzo kwa wanataaluma pamoja na vifaa vya kufundishia na kujifunzia kwenye maabara zetu” aliomba Dkt. Hosea.

Awali Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Prof. Raphael Chibunda amesema mchango wa miradi hiyo miwili ya SACIDS na (ACE IRPM & BTD iliyofadhiliwa na Benki ya Dunia ni mkubwa sio tuu kwa Tanzania bali kwa bara la Afrikakwani  tafiti zake zinagusa Afrika.

“Naomba nitumie nafasi hii kushukuru sana msaada tunaoupata kutoka Serikali yetu na Bank ya Dunia ambayo inasaidia chuo kwenye kutekeleza majukumu yake na kupitia Mradi wa HEET tunawekeza katika shamba letu la Miti huko Madaba ili ndani ya kipindi cha miaka mitano tuongeze mapato yetu ya ndani ya Chuo na kupunguza utegemezi” alisema Prof. Chibunda.

Katika mkutano huo Chuo kilipata nafasi ya kutoa mawasilishao mbalimbali ikiwemo Historia, Kazi na mafanikio ya Chuo toka kuanzishwa kwake iliyowasilishwa na Naibu Mkamu Mkuu wa Chuo Taaluma Utafiti na Ushauri wa Kitaalamu Prof. Maulid Mwatawala ambaye alieleza namna Chuo kinavyotekeza majukumu yake.

Aidha, Mawasilisho mengine ni Utekelezaji wa Taasisi ya afya moja inayoshughukikia magonjwa ambukizi kusini mwa jangwa la Sahara (SACIDS) lililowasilishwa na Prof. Gerald Misinzo, Wasilisho la Mradi wa HEET lililowasilishwa na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Mipango Utawala na Fedha Prof. Amandus Mharwa na Mratibu wa Mradi huo Dkt. Winfred Mbungu na Wasilisho la  Kituo cha Umahiri cha Mashariki na Kusini mwa Afrika cha Kudhibiti Panya na matumzi yake kanitika kunusa (ACE IRPM & BTD kutoka kwa Prof. Appiah Masawe.

Baada ya mawasilisho hayo Mkurugenzi huyo Mkazi wa Benki ya Dunia Nchini Tanzania Bw. Nathan Belete pamoja na ujumbe wake walipata nafasi ya kutembelea kuona vituo hivyo na kazi zinazofanyika na kuona namna fedha walizotoa zilivyosaidia kufanyika kwa tafiti zenye faida kubwa kwa taifa na Afrika. 


Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Prof. Raphael Chibunda  akitoa salamu za SUA.

Prof. Gerald Misizo akitoa wasilisho kuhusu utekelezaji wa Taasisi ya afya moja inayoshughukikia magonjwa ambukizi Kusini mwa Jangwa la Sahara (SACIDS) 

Prof. Appiah Masawe akiwasilisha Utekelezaji wa mradi kwenye Kituo cha Umahiri cha Mashariki na Kusini mwa Afrika cha Kudhibiti Panya na matumzi yake kanitika kunusa (ACE IRPM & BTD)

Mratibu wa Mradi wa HEET Dkt. Winfred Mbungu akiwasilisha utekelezaji wa Mradi huo SUA.

Kaimu Mkurugenzi wa Elimu ya Juu, Dkt Keneth Hosea akitoa salamu za Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia.

Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Nchini Tanzania Bw. Nathan Belete akizungumza mara baada ya kusikia mawasilisho yote ya miradi inayofadhiliwa na Benki ya Dunia.


 Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Mipango Utawala na Fedha Prof. Amandus Mharwa akiwasilisha sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa HEET.




Naibu Mkamu Mkuu wa Chuo Taaluma Utafiti na Ushauri wa Kitaalamu Prof. Maulid Mwatawala akitoa salamu na Historia ya Chuo.


Post a Comment

0 Comments