SUAMEDIA

Hospitali ya Rufaa ya Wanyama yageuka nuru ndani, nje ya mipaka ya Tanzania

 

Na: Farida Mkongwe

Hospitali ya Rufaa ya Wanyama iliyopo katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) imekuwa ni msaada mkubwa kwa wanyama wanaougua magonjwa sugu yanayoshindikana kutibiwa katika kliniki mbalimbali nchini.


Prof. Mshiriki kutoka Ndaki ya Tiba ya Wanyama na Sayansi za Afya Claudius Luziga akiwa kwenye Maonesho ya Vyuo Vikuu yanayofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar Es Salaam. Picha na Asifiwe Mbembela

Kauli hiyo imetolewa Julai 20, 2023 na Prof. Mshiriki kutoka Ndaki ya Tiba ya Wanyama na Sayansi za Afya Claudius Luziga akiwa kwenye Maonesho ya Vyuo Vikuu yanayofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar Es Salaam wakati akizungumza na SUAMEDIA kuhusu huduma zinazotolewa na hospital hiyo.

Prof. Luziga amesema hospitali hiyo inatoa huduma za juu zaidi ikiwemo kupiga X-ray ambazo ni zile za digitali ili kujua tatizo alilonalo mnyama, huduma za kuboresha wanyama ikiwemo uhimilishaji na huduma kama Utra Sound na upasuaji mkubwa ambao hauwezi kufanyika katika kliniki ndogo ndogo.

“Wanyama huwa wanakuja Hospital ya Rufaa au wakati mwingine tunawafuata kule kwenye mazizi pale inapotokea dharura labda wanyama wanakufa wengi basi wakulima wanatoa taarifa na wataalamu wetu wanawafuata”, amesema Prof. Luziga.

Amesema kuwa wananchi wakifika kwenye banda la SUA lililopo ndani ya viwanja hivyo watapata elimu ya kutosha kuhusu huduma zinazotolewa na Hospital hiyo na kwamba sasa wafugaji hawana sababu tena ya kuangaika au kuwa na hofu kuhusu matibabu makubwa ya wanyama wao.


Post a Comment

0 Comments