SUAMEDIA

Wilaya ya Kilombero yaiomba SUA kusaidia mbinu za kuongeza thamani na uzalishaji wa Mpunga.

 Na: Amina Hezron,Kilombero.

Mkuu wa Wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro Dunstan Kyobya amewaomba Wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kujenga uelewa wa namna sahihi ya kuongeza thamani ya zao la mpunga pamoja na mbinu za kuongeza tija katika uzalishaji wa zao hilo katika Wilaya hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Mhe. Dunstan Kyobya akizungumza na wadau wa kilimo pamoja na wataalamu kutoka SUA.

Kyobya ametoa maombi hayo wakati alipokuwa akifungua Warsha iliyoandaliwa na Watafiti kutoka SUA iliyokutanisha wadau wa kilimo kwaajili ya kutoa mrejesho wa utafiti uliohusu Utayarishaji Shirikishi wa Huduma za Hali ya Hewa ili Kuboresha Uhakika wa Chakula, Lishe na Afya nchini Tanzania.

Amesema bado hajaridhishwa na kiwango cha uzalishaji wa mpunga katika wilaya yake japokuwa ndiyo wilaya inayoongoza katika uzalishaji wa zao hilo ambapo Halmashauri ya wilaya ya Mlimba peke yake ikizalisha vyema inauwezo wa  kulisha Tanzania nzima hivyo amewataka wataalamu kutoka SUA kuelekeza njia sahihi na mbegu bora za kutumika.

“Tunalima tunapata kidogo heka moja ya shamba la mpunga linaweza kuzalisha gunia 25 lakini nimesoma sehemu wakati nakuja huku kuwa unaweza kuzalisha mpaka gunia arobaini na tano hadi hamsini za mpunga kwanini na sisi tusifanye hivyo”, alisema Kyobya.

Akielezea lengo la warsha hiyo na kuanzishwa kwa Mradi huo Kaimu Mratibu wa Mradi kutoka SUA  Dkt. Sylvester Haule amesema ni kuongeza matumizi ya huduma za hali ya hewa kwa kujifunza jinsi mabadiliko ya hali ya hewa yanavyoathiri kilimo, mifumo ya chakula na afya pamoja na mienendo ya maamuzi katika ngazi ya kaya.

Kaimu Mratibu wa Mradi kutoka (SUA) Dkt. Sylvester Haule akiuelezea Mradi kwa Mkuu wa Wilaya ya Kilombero.

“Katika Mradi wetu huu tumelenga kuongeza uwezo wa mamlaka ya hali ya hewa kutoa tabiri zinazokidhi mahitaji ya wakulima, kuboresha huduma za hali ya hewa na uwasilishaji wake kwa wadau katika ngazi ya chini kwa kushirikiana na Mamlaka za hali ya hewa,Wizara ya Kilimo, Wizara ya  Afya na Maafisa ugani na Maafisa afya”, alifafanua Dkt Haule.

Mradi huu wa miaka miwili umekuwa ukitekelezwa kuanzia mwezi Aprili 2021, na kumalizika 2023 katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba na na  Mvomero  kwa ushirikiano baina ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Taasisi ya Michelsen (CMI) ya nchini Norway, Kituo cha Kimataifa cha Utafiti wa Tabianchi na Mazingira (CICERO) ya Norway, kituo cha Utafiti cha Norway (NORCE)  Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)  na Taasisi nyinginezo zilizoko Norway.


Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Mhe Dunstan Kyobya na Wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA.


Viongozi mbalimbali wa Wilaya na Wadau wengine wa  kilimo wakisikiliza mawasilisho ya mtokeo ya utafiti.

Viongozi mbalimbali wa Wilaya na Wadau wengine wa  kilimo wakisikiliza mawasilisho ya mtokeo ya utafiti.

Viongozi mbalimbali wa Wilaya na Wadau wengine wa  kilimo wakisikiliza mawasilisho ya mtokeo ya utafiti.

Viongozi mbalimbali wa Wilaya na Wadau wengine wa  kilimo wakisikiliza mawasilisho ya mtokeo ya utafiti.


 

 

 

 

 

 

 

Post a Comment

0 Comments