Na Gojo Mohamed
Ushirika wa wahitimu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUGECO)
umeendelea kuwapatia vijana fursa kwa kuwapeleka nchi mbalimbali Duniani
ikiwemo Denmark, kwa ajili ya mafunzo ya utarajali ili kuwaongezea ujuzi na
maarifa katika sekta ya Mifugo.
Dkt. Othaman Mohamed akimkabidhi cheti na tiketi ya Ndege Bi. Phinna Ngowi anayeelekea nchini Denmark kwa ajili ya mafunzo
Hayo yamebainika katika hafla fupi iliyofanyika Januari 9,
2023 Makao Makuu ya Ushirika huo Mkoani Morogoro ambayo imehudhuriwa na Uongozi
wa SUGECO pamoja na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa ajili ya
kuwaaaga baadhi ya vijana wanaotarajia kwenda nchini Denmark hivi karibuni.
Kwa upande wake Dkt. Othaman Mohamed kutoka Wizara ya Elimu
Sayansi na Teknolojia, ameipongeza SUGECO na kuongeza kuwa Wizara hiyo inaunga
mkono juhudi zinazofanywa na Ushirika huo, kwani vijana hao watakaporudi nchini
mara baaada ya mafunzo wataleta chachu ya maendeleo na mabadiliko katika sekta
ya Mifugo nchini.
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya SUGECO Dkt. Anna Temu amesema kuwa
zoezi hilo lilianza kwa kuwapeleka vijana kupata ujuzi nchini Israeli na Marekani
lakini kwa sasa wanawapeleka vijana katika nchi ya Denmark na wataendelea
kuwapeleka katika nchi zingine, na ameongeza kwa kuwakaribisha vijana SUGECO
ili kupata ujuzi hasa katika maswala ya kilimo pamoja na mifugo.
Baadhi ya wahitimu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo kutoka Usharika wa SUGECO wakiwa katika hafla fupi ya kuagwa
Kwa upande wake Ibrahimu Hassan ambae ni miongoni mwa vijana
wanaotarajia kwenda nchini Dermak kwa ajili ya mafunzo ya utarajali, amesema
kuwa matarajio yake ni kupata ujuzi kwa ufanisi zaidi ili kuwasaidia vijana
wenzake kutokana na ujuzi huo, pia ameshukuru kwa kupata fursa hiyo na kuupongeza uongozi wa SUGECO kuhusani katika program.
Mafunzo hayo ya utarajali yatakuwa kwa muda wa miezi kumi na
nane 18 kwa vijana kujifunza na kupata ujuzi katika sekta Ufugaji na
wanatarajia kupeleka vijana 56 nchini Denmark kwa mwaka huu.
0 Comments