NA:Winfrida Nicolaus
Idara ya Teknolojia ya Chakula
na Uchakataji wa Mazao ya Shambani iliyopo katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA inatoa Elimu ya namna ya kubadilisha mazao ya shamba kuwa katika
bidhaa zenye thamani kibiashara na hivyo kuwawezesha wakulima kukua uchumi.
Ameelezea hayo Fundi Sanifu Maabara kutoka Idara hiyo Bw.
Tamambele Masinga wakati akizungumza na SUAMEDIA kwenye Maonesho ya 29 ya
Wakulima, Wafugaji na Wavuvi Kanda ya Mashariki yanayofanyika mkoani Morogoro.
Amesema kile wanachofanya ni
kujaribu kubadilisha Mazao ya Shamba kuwa katika Bidhaa bora hivyo
wanayaongezea thamani mazao hayo ili yaweze kuwa na muda mrefu ambapo
Mwanafunzi anajifunza kutazama mazao ya Shamba katika bidhaa tofauti tofauti za
kibiashara na kuweza kujikwamua kiuchumi.
Bw. Masinga amesema
anawahamasisha wananchi kupitia Mafunzo mbalimbali ya muda mfupi kwa faida yao
wenyewe kwasababu wale ambao wanapata ujuzi kama wa Uchakataji wa Mazao kama
vile Matunda kwaajili ya Juice, Vinegar
pamoja na Wine au Usindikaji wa Mbogamboga
watasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza uharibifu wa Mazao ya Shamba ambayo
yangeweza kuharibika kama yangeachwa bila kubadilishwa au kuyaongezea thamani.
Aidha amesema vitu ambavyo
wanafunzi wameweza kufanikiwa kuvitengeneza kupitia usimamizi mzuri wa Wataalam
wa Maabara na wanavionesha katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki kwa
mwaka huu wa 2022 ni pamoja na Chili source
ambayo imetokana na Karoti, na Nyanya, Tomato
Source pamoja na Mkate uliotengenezwa kwa Unga wa Viazi Lishe, Maharage ya
Soya na Ngano ambayo haijakobolewa.
“Hivyo vitu ambavyo tumekuja
kuhamasisha Wananchi ni kuwashauri kupitia short
course au Mafunzo ya muda mfupi wakaweze kujifunza vizuri Zaidi mfano
tunafanya uchakataji wa Matunda ambapo tunatengeneza Juice, Charm, Vinega pamoja na Wine
kwa hiyo ni vitu ambavyo tunajifunza mbali na hapo pia tunafanya usindikaji wa
mbogamboga”, amesema Bw. Masinga
“Na hapa tumekuja na chili souce ambayo imetengenezwa kwa
karoti, nyingine ya nyanya pia tuna mkate wa lishe ambayo umetengenezwa kwa
Ngano ambayo haijakobolewa, maharage ya soya hii yote ni kuhakikisha mtumiaji
anapata virutubisho ambavyo ni vizuri vilevile
tunamwambia mwananchi tunatoa Elimu ya muda mfupi na kwa bei nafuu, hivyo wiki
moja, tatu au mwezi mmoja anapata elimu yake na kujikwamua kiuchumi”.amesisitiza
Bw. Masinga.



0 Comments