SUAMEDIA

Bidhaa zilizofanyiwa utafiti kuoneshwa Banda la SUA katika Maonesho ya 29 Nanenane Morogoro

 NA:Winfrida Nicolaus

Wananchi wa Morogoro na Kanda ya Mashariki wametakiwa kutembelea banda la SUA kwenye Maonesho ya 29 ya Wakulima, Wafugaji na Wavuvi ili kujifunza na kujionea baadhi ya Bidhaa ambazo zimefanyiwa Utafiti kutoka kwenye Miti na kutengeneza dawa ambazo zinatibu Magonjwa ya aina mbalimbali.





Amesema hayo Mtaalam wa Maabara kutoka Idara ya Fiziolojia, Biokemia na Famakolojia, Ndaki ya Tiba ya Wanyama na Sayansi ya Afya katika Chuo cha Sokoine cha Kilimo SUA Bw. Ignatus Kiiza wakati akizungumza moja kwa moja na SUA Radio kutoka kwenye Viwanja vya Maonesho hayo.

Amesema kuna aina mbalimbali za dawa ambazo zimetoka kwenye miti ambayo imefanyiwa utafiti na kuweza kutibu magonjwa endapo mtu akitumia kwa usahihi anaweza kupona kabisa ambapo dawa hizo ni pamoja na Wound Spray ambayo kazi yake kubwa ni kutibu Vidonda vipya, vidonda vilivyotokana na magonjwa kama ya Kisukari, vilivyotokana na Moto na vile ambavyo vimekaa muda mrefu.

Bw. Kiiza amesema aina nyingine ya dawa inaitwa Wound Gell ambayo ipo kwenye mfano wa mafuta na kazi yake kubwa ni kutibu Magonjwa ya Ngozi yaani Fungus, Mapunye au Mashiringi pamoja na harara hivyo mtu mwenye matatizo kama hayo akipata dawa hizo zitamsaidia kwa muda mfupi na kumuwezesha kupona kabisa.

Vilevile kuna sabuni ambayo inatumika kama dawa  kwa njia ya kuogea ambapo mtu anaweza kuitumia kwa kutibu Magojwa ya Ngozi na kuilinda Ngozi yake .

“Kuna Product yaani bidhaa za dawa ambazo zimetokana na miti ambayo imefanyiwa utafiti na dawa hizo zinaweza kutibu magonjwa ya aina mbalimbali kama vile vidonda vya muda mrefu au vipya, vidonda vya moto na vile kama mtu wa kisukari akipata hivyo kuna dawa iitwayo Wound Gelly ambayo mtu akiitumia anapona kwa muda mfupi”, ameeleza zaidi Bw. Kiiza.

Aidha Bw. Kiiza amewataka watanzania kutembelea banda la SUA kwenye Maonesho hayo ya 29 ya Wakulima, Wafugaji na Wavuvi kujipatia bidhaa hizo lakini pia kutembelea chuo cha SUA kutoka Idara ya Fiziolojia, Biokemia na Famakolojia ili wajipatie dawa hizo na kupatiwa elimu kuhusiana na namna bora ya kuzitumia pamoja na faida zake.


 

 

Post a Comment

0 Comments