NA: Winfrida Nicolaus
Chuo Kikuu cha Sokoine cha
Kilimo SUA kupitia Taasisi ya Kuthibiti Viumbe Hai Waharibifu inatoa Elimu
kuhusiana na Teknolojia rahisi na Rafiki kwaajili ya kudhibiti Viumbe Hai Waharibifu
hasa Panya katika Maonesho ya 29 ya Wakulima, Wafugaji na Wavuvi Kanda ya
Mashariki.
Amesema hayo Mtafiti Msaidizi kutoka
Taasisi hiyo Dkt. Amina Ramadhani Issae wakati akizungumza Mubashara kupitia
SUA Radio kutoka katika Viwanja vya Maonesho ya 29 ya Wakulima, Wafugaji na
Wavuvi Kanda ya Mashariki.
Amesema katika maonesho hayo
wanaonesha Teknolojia mbalimbali za kudhipiti Viumbe Hai Waharibifu kama Panya
ikiwemo Teknolojia ya kutumia Bundi katika kudhibiti Panya Shambani, Mitego ya
aina mbalimbali ya kutegea panya ambayo inatengenezwa na Taasisi hiyo lakini
pia Teknolojia ya Kudhibiti Panya Majumbani ikiwemo Mbinu ya kutumia Mkojo wa
Paka kwaajili ya kufukuza Panya ndani ya nyumba.
Dkt. Amina amesema licha ya wananchi
kuona Teknolojia mbalimbali za kudhibiti Panya vilevile wanaelimishwa kuhusiana
na Madhara ya Panya katika kusambaza Magonjwa kwa binadamu na hata Wanyama
wengine lakini pia Panya haohao licha ya kusababisha madhara wamekuwa na faida
kama vile kuokoa Maisha ya Binadamu ikiwemo kugundua Vimelea vya Magonjwa kama
TB, Kugundua Mabomu yaliyotegwa Ardhini Pamoja na kutambua harufu za binadamu
waliofukiwa na vifusi.
Amesema Bundi ana uwezo wa kula
Panya mmoja hadi kumi na mbili kwa siku hivyo katika kudhibiti Panya kwa
kutumia Bundi anachotakiwa kufanya Mkulima ni kutengeneza mazingira Rafiki
yanayomuwezesha bundi kutua katika shamba lake ikiwemo kutengeneza viota vya
mbao vyenye tobo na kuvining”iniza kwenye nguzo ambapo vitamuwezesha bundi huyo
kutua na kukabiliana na panya katika shamba lake.
“Katika
banda la SUA Taasisi ya Kudhibiti Viumbe Hai Waharibifu kuna mambo mbalimbali
hasa Teknolojia ya Kuthibiti Panya Mashambani vilevile kuwaeleza wananchi au
watu wanaotembelea banda letu Madhara ya Panya lakini kama chanzo cha kusambaza
Magonjwa kwa binadamu na hata wanyama wengine lakini wamekua na faida nyingi
licha ya kusababisha majanga kuna wanaosave
Maisha ya binadamu mfano Panya wanaogundua Vimelea vya Magonjwa kama TB ”,
amesema Dkt. Amina .
“Pia kuna Panya ambao wanaweza
kugundua Mabomu yaliyotegwa Ardhini na ambao wamefundishwa kuokoa watu ambao
wamepata Majanga kama vile kuangukiwa na vifusi au magorofa sasa kuna wale
Panya ambao wamefundishwa jinsi ya kutambua harufu ya binadamu ambao wamenasa ndani
ya vifusi”, ameongeza Dkt. Huyo.
Aidha lengo la kuja kwenye
Maonesho hayo ya 29 ya Wakulima, Wafugaji na Wavuvi ni kuwaelimisha wananchi
hivyo amewasisitiza kutembelea Banda la SUA hasa katika Taasisi ya Kuthibiti
Viumbe Hai Waaribifu kujifunza ili waweze kudhibiti viumbe hao bila ya kutumia
kemikali.




0 Comments