SUAMEDIA

Wakulima wa mbogamboga na matunda watakiwa kulima kwa kufuata kanuni bora za kilimo 1


Na.Vedasto George.

Wakulima wa mbogambona na matunda wametakiwa  kuendesha kilimo hicho kwa kufuata kanuni bora za kilimo ili waweze kuzalisha kwa tija  na kuweza kushindana kwenye soko la ndani na nje ya nchi.

Wito huo umetolewa na Katibu Tawala mkoa wa Morogoro Bi. Mariam Mtunguja wakati wa  ufungaji wa Mradi wa miaka mitano na nusu  wa FEED THE FUTURE TANZANIA MBOGA NA MATUNDA ambapo  umewezesha kutoa mafunzo kwa wakulima wa mboga mboga na matunda zaidi  ya 180,000 kutoka wilaya nne za mkoa wa Morogoro .

‘Tuzalishe lakini tuzalishe kibiashara lakini tuhakikishe pia tunazalisha kwa tija  yaani kama unatakiwa kufuata taratibu za kanuni bora za kilimo ni sasa na hii itatusaidia kuacha kuzalisha kiolela na mazao ya ovyo ambayo ayawezi kuingia sokoni  ,huu mradi  umewezesha wakulima wetu 183,709 ambao wamepata mafunzo mbalimbali juu ya ulimaji wa mazao ya mboga mboga na matunda”, amesema Bi. Mariam. 

Aidha Mtunguja amewaagiza Wakurugenzi wa halmashauri ambazo zimenufaika na Mradi wa mboga mboga na matunda kuendelea kutenga bajeti kwa maafisa ugani ili waweze kuendelea kutoa elimu kwa wakulima ikiwemo kuwawezesha kupata mbegu bora ambazo zitaweza kutoa mazao yenye tija kwa mkulima.

Pia ameongeza kuwa serikali imeendelea kuchukua jitahada za makusudi  za kutafuta masoko nje ya nchi ili wakulima wanaozalisha mazao yao kutoka shamba  waweze kupata soko la uhakika.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa FEED THE FUTURE TANZANIA MBOGA NA MATUNDA, Antonio Coello  amesema Mradi huo umetekelezwa  kwa mafanikio makubwa katika wilaya 26 za mikoa ya Morogoro, Mbeya, Songwe,Iringa na Njombe  na wilaya 10 za Tanzania Visiwani katika visiwa vya Unguja na Pemba.

“Mradi unatumia mfumo wa kushirikisha wadau mbalimbali  ili kuweza kutoa huduma za kilimo bora ,Teknolojia za kilimo  pamoja na elimu  ya lishe  ili kuweza kuwafikia watanzania maelfu kwa maelfu  wanaoshiriki katika mnyororo wa thamani katika uzalishaji wa mazao ya mboga mboga na matunda”,  amesema Mkurugenzi huyo

 Naye Mkurugenzi Msaidizi  na Mwalishi wa USAID Stephen Mruma ameeleza mafanikio  mbalimbali yaliyofikiwa na Mradi huo  tangu kuanzishwa kwake mwaka  2017 hadi sasa ambapo umefikia tamati mwaka 2022.

Mruma  amesema Mradi huo wa Mbogambona na Matunda umeweza kuwafikia watu zaidi ya 400,000 kwa Tanzania nzima na wote wamefundishwa  kanuni bora za kilimo cha mboga na matunda ikiwemo kutafutiwa masoko ambayo  wakulima wataweza kuuza mazao yao na kuweza kupata kipato cha kuendeleza familia zao.

Nao wakulima ambao ni wanufaika wakubwa wa mradi huo akiwemo Abel Mchome pamoja na Anania Masimile kutoka Kampuni ya Balton Tanzania wamesema kwa kipindi chote cha miaka mitano na nusu Mradi umekuwa ukiwaunganisha na wadau mbalimbali ikiwemo Taasisi za fedha , Wauza pembejeo za kilimo na Wafanyabiashara wakubwa ambao wamekuwa wakinunua bidhaa zao  .

“Tumenufaika sana na mradi huu kwanza walipokuja walitupa elimu na njia bora za kufanya kilimo cha mboga na matanda na sisi tukaanza kulima tuliona mafanikio mazao yalitoka mengi baada ya kuzalisha ikabidi watutafutie soko na kutuunganisha wa taasisi za fedha kwa ajili ya kutuwezesha kupata mikopo, kwa kweli mradi huu unaisha lakini maarifa tuliyopewa tutayaendeleza”,alisema Abeli Mchome mkulima wa Mboga na matunda kutoa Halmashauri ya wilaya ya kilosa.

Katika Video

https://www.youtube.com/watch?v=kHnwFtUZ2GY




Post a Comment

0 Comments