SUAMEDIA

Kufuata Sheria, Kanuni, Taratibu, Miongozo kuepuka Doa litakalochafua Chuo - Prof. Mwatawala

NA, Hadija Zahoro

Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA),  kimefungua mafunzo ya siku mbili kwa watumishi wote ,kwa lengo la kuwakumbusha kutekeleza majukumu yao kwa kufuata sheria, kanuni taratibu  na miongozo inayotolewa na serikali pamoja na Chuo  katika kipindi chote cha utekelezaji wa majukumu hayo chuoni hapo.

Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaalamu Prof. Maulid Mwatawala akimwakilisha Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Rafael Chibunda katika Mafunzo ya siku mbili kwa watumishi wote ,kwa lengo la kuwakumbusha kutekeleza majukumu yao kwa kufuata sheria, kanuni taratibu  na miongozo inayotolewa na serikalia

Mafunzo hayo yaliyoandaliwa  SUA, yameanza tarehe 12 Aprili  na kukamilika Aprili 13, 2022 katika ukumbi wa Multipurpose uliopo chuoni hapo, yanayowahusisha Wanataaluma wakiwemo Wakuu wa Idara na watumishi  wote pamoja na  Wasimamizi  wa Miradi ya Utafiti SUA.

Akimwakilisha Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Rafael Chibunda, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaalamu Prof. Maulid Mwatawala amesema Wakuu wa Idara  zote, wanahusika moja kwa moja  na mafunzo hayo kwa sababu wanasimamia na kuwezesha  tafiti mbalimbali.

Amesema kwa kuonesha umuhimu wa mafunzo hayo, wamesimamisha  masomo  ndani ya siku hizo mbili  kwa masomo ya asubuhi chuoni hapo, hivvo amewaomba wakuu hao wa idara kuwakumbusha wanataaluma wote kushiriki kikamilifu katika mafunzo hayo.

Ameongeza kuwa mafunzo hayo  yanagusa mambo muhimu yakiwemo usimamizi na matumizi ya pesa za miradi,usimamizi na uendeshaji wa miradi ya utafiti chuoni,  utunzaji wa kumbukumbu za miradi, utekelezaji  wa miradi ya maendeleo inayotokana na utafiti , utekelezaji wa shughuli za ununuzi masuala ya afya na namna ya kuzingatia  sheria za miongozo ya serikali  na chuo katika mikataba husika ili kuepuka matatizo yatakayokikumba chuo na kufanya watatifi kushindwa kukamilisha kazi zao. 



Aidha, Prof. Mwatawala amesema  kuwa suala la kufuata sheria, kanuni, taratibu na miongozo,  litaisaidia chuo kuepuka hoja za kikaguzi zitakazoibuliwa na   wakaguzi wa ndani na wale wa nje katika  maeneo ya usimamizi wa miradi ya chuo na kukiingiza chuo katika matatizo makubwa ambayo yataleta doa litakaloichafua  na kufunika kazi zote nzuri zitakazofanywa chuoni hapo.

‘‘Ndugu washiriki wa mafunzo kama nilivyoseam kufuata sheria,kanuni  na taratibu kutatusaidia sana kuepuka hoja  mbalimbali za kikaguzi na kukiingiza chuo katika matatizo makubwa, kwa sababu tunapokuwa na hoja hizo za kikaguzi  hata tukitekeleza majukumu yetu mengine kwa ufanisi wa hali ya juu bado kunakuwa na doa kubwa , yani hilo doa linakuwa linafunika kazi zetu nzuri ambazo tumefanya  hata kama tulifanya uzinduzi, uvumbuzi  wa aina yoyote, lakini kwa kutofuata sheria na taratibu tunaweza kufunikwa na kuingia katika doa hilo’’. Amesema Prof. Mwatawala.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Kudhibiti Viumbe Hai Waharibifu ambaye ni mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo, Prof. Loth  Mulungu amesema kituo hicho kina hakikisha kinatoa  matokeo ya tafiti yenye asili ya SUA kwa ajili ya kutatua matatizo katika jamii. 

Ametolea mfano njia ya kutatua matizo ya panya kuharibu mazao hivyo wanafanya majaribio ya  kutengeneza bidhaa kwa kutumia mkojo wa paka  ili kuwafanya panya hao kuhisi uwepo wa paka na kupelekea kuogopa kuharibu mazao hayo.








Post a Comment

0 Comments