Na Gladness Mphuru
SUA
Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimesema ili nchi iweze kupanga na kutenga bajeti kulingana na idadi ya wahitaji, kwenye sekta mbalimbali kama sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi kujua uhitaji wa wakulima na katika sekta ya Elimu ni muhimu watu wakajitokeza katika zoezi la sensa
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) Prof. Raphael Chibunda akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani ofisini SUA-MorogoroHayo yamesemwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) Prof. Raphael Chibunda Aprili 20, 2022 ofisini kwake Kampasi ya Edward Moringe Sokoine mkoani Morogoro, wakati akizungumza na waandishi wa habari kwa lengo la uhamasishaji wa zoezi la Sensa ya Watu na Makazi linalotarajiwa kuanza Agosti 23, mwaka huu.
“Kama ambavyo mheshimiwa Rais mama yetu Samia Suluhu
Hassan amekuwa akihimiza hakuna kitu muhimu kama zoezi hili, na hili sio la
Tanzania pekee ni zoezi linalofanyika katika kila nchi duniani kwa vipindi
mbalimbali walivyojipangia ili kuweza kupata takwimu sahihi kwenye kupanga
maendeleo ya nchi husika” Amesema Prof. Chibunda
Ametoa wito kwa watanzania wote hususan kwa wanajumuiya wa SUA
wafanyakazi na wanafunzi hasa vijana ambao wanashiriki zoezi hili kwa mara ya
kwanza kushiriki kikamilifu kwa sababu ndio nguvukazi kubwa kwa taifa.
“Na vilevile nishauri katika baadhi ya jamii za nchi
yetu kumekuwa na tabia ambazo sio nzuri na potofu walemavu wa viungo wamekuwa
hawatolewi hadharani ili nao waweze kuhesabiwa, ni muhimu watu wote kuhesabiwa
hususani wenye mahitaji maalumu ijulikane ni wangapi ili nchi iweze
kuwahudumia”
Prof. Raphael Chibunda, amesema yeye yuko tayari pamoja na
familia yake kushiriki katika zoezi muhimu la sensa ya watu na makazi, zoezi
litakalo rahisishia nchi kupanga mipango ya maendeleo.
Kauli mbiu ya Sensa ya watu na makazi kwa mwaka 2022 inasema “Sensa
ni msingi wa mipango ya maendeleo shiriki kuhesabiwa tuyafikie maendeleo ya
Taifa”
0 Comments