SUAMEDIA

Vijana zaidi ya 300 Manispaa ya Morogoro wanufaika na mafunzo SUA

Na Gerald Lwomile

Morogoro

Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kupitia Taasisi ya Elimu ya Kujiendeleza (ICE) kimefanikiwa kuwafundisha zaidi ya vijana 300 kutoka Kata tisa ikiwemo Kilakala na Boma mafunzo ya uoteshaji na uzalishaji wa miti ya matunda kibiashara, ufugaji wa kuku, ufugaji wa samaki na ujasiriamali

Hayo yamesemwa mkoani Morogoro na Mkuu wa Kitengo cha Ugani ICE-SUA Dkt. Innocent Babili wakati akizungumza na SUA Media mapema wiki hii ili kujua ni kwa namna gani wazalishaji wa miche ya matunda wamenufaika na mafunzo hayo

Dkt. Babili amesema katika mafunzo ambayo wameyatoa hivi karibuni vijana mbalimbali kutoka kata ya Kilakala na Boma wamejifunza namna bora ya kuotesha na kuzalisha miche ya matunda kibiashara

“Mafunzo haya ni moja ya majukumu ambayo ICE imefanya kwa mwaka 2021/2022 lakini pia tumekuwa tukitoa mafunzo ya aina mbalimbali kama ufugaji wa kuku na ufugaji wa Samaki na hata watafiti na hii inadhihirisha kuwa SUA ni hazina ya kilimo” amesema Dkt. Babili

Wakizungumzia mafunzo hayo vijana Evarist Luvanda na Suzan Fabian wakazi wa mtaa wa Mahedu kata ya Kilakala Manispaa ya Morogoro wamesema mafunzo hayo yamewasaidia katika kufuhamu mambo mbalimbali kama ujasirimali, uoteshaji na uzalishaji wa miche ya matunda

“Mimi nimejifunza mambo mengi sana ambayo awali sikuyajua nimejifunza namna ya uoteshaji wa miche na ubebeshaji kitaalamu wanaita ‘budding’ na unaweza kubesha mfano mlimao kwa mchungwa” amesema Suzan

Mafunzo hayo yametolewa na SUA kwa kushirikiana na SWISSCONTACT na Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, mbali na vijana hao kupata mafunzo lakini pia wamepata vyeti ambayo vimethibitisha ushiriki wao






Post a Comment

0 Comments