SUAMEDIA

Ukuaji bora wa Samaki kutegemea matunzo na usafi wa maji

 

Na Flora Rugaimukamu

DSJ

Chuo cha Kilimo cha Sokoine (SUA)  kimesema kitaendelea kutoa elimu ambayo itawasaidia wafugaji wa samaki kujua namna ya kuwatunza na namna ya kuwapa virutubisho ambavyo vitasaidia ukuaji wa viumbe hao.

Akizungumza na SUAFM 101.1 leo Machi 09, 2022 Mhadhiri Msadizi kutoka Kitengo cha Ukuzaji wa Viumbe SUA Bi. Mariam Bakari amesema ili kusaidia ukuaji bora wa samaki mfugaji anatakiwa kuhakikisha samaki wanapata matunzo bora hasa usafi wa maji ambayo ndiyo makazi ya viumbe hao na kupata vyakula vyenye virutubisho ambavyo  vitasaidia katika ukuaji wao.

Amesema vyakula vyenye virutubisho kwa samaki husaidia katika ukuaji bora wa viumbe hai, na kuongeza kuwa virutubisho hivyo vinakuwa na  protini, wanga, vitamini na madini pia ameshauri samaki kupata mwanga wa jua ambao husaidia kuzalisha chakula cha asili.

"Samaki ili kuweza kukua wanahitaji vyakula vyenye virutubisho vyote ambavyo vimegawanyika katika makundi mbalimbali, chakula kimojawapo ni chakula asili ambacho hiki upatikana ndani ya maji" amesema Bi Mariam Bakari

Hata hivyo mtaalamu huyo amewataka wafugaji kuwa makini katika ulishaji wa samaki na pia umakini katika usafi maji na kuwa ni muhimu kubadili maji pindi yanapokuwa machafu ili kuzuia vifo vya samaki.

"Ningependa kutoa ushauri wafugaji wa samaki kuwa makini hasa katika upande wa chakula ili kuwezesha samaki kukua wanatakiwa kupata vyakula vyenye virutubisho vyote na ili kuepusha vifo vya samaki ni muhimu kuhakikisha samaki wanaishi katika maji masafi na kipindi cha mvua tunashauri mfugaji kutengeneza uzio ambao utazuia maji machafu kufika katika makazi ya viumbe hao” amesema Bi. Mariam





Post a Comment

0 Comments