Gerald Lwomile
Mazumbai - Tanga
Imeelezwa kuwa kuwepo kwa rushwa nchini kwa kiasi
kikubwa kumeongeza umaskini katika jamii kwa kuharibu mifumo ya kiuchumi na
kupunguza uwezo wa serikali kukusanya mapato ambayo hutumika kuwahudumia
wananchi
Mbangula amesema rushwa imekuwa ikiharibu mifumo ya
elimu na hatimaye kuzalisha taifa lenye watu wajinga lakini pia huduma za afya
zimekuwa zikizorota na hatimaye kiwango cha maradhi kwenye jamii kuongezeka
“Ikumbukwe kuwa nchi yetu ipo vitani na vita yetu ni
dhidi ya maadui watatu wakubwa ambao ni Umaskini, Ujinga na Maradhi. Rushwa
imekuwa ikiongeza ugumu wa kupambana na maadui hawa” amesema Mbangula
Akizungumzia namna ya kupambana na rushwa katika
utumishi wa umma amesema ni muhimu kila mtumishi wa umma kutambua nafasi adhimu
aliyonayo kwani watumishi wa umma ndiyo taasisi iliyokasimiwa wajibu na
serikali wa kuratibu na kusimamia shughuli zote za utoaji huduma na maendeleo
Awali akifungua mafunzo hayo Kaimu Msimamizi wa Misitu
wa Mazumbai Bw. Chamahndi Bigingo Muriga amesema SUA kupitia KKU imeandaa
mafunzo haya ili kutoa uelewa kwa watumishi kuhusu uadilifu na jinsi ya
kupambana na rushwa, na namna ya mtumishi kuenenda kama mtumishi wa umma ili
kuleta tija na ufanisi wakati wa kutekeleza majukumu yake.
Amesema Menejimenti ya Chuo
itaendelea kuandaa mafunzo kama haya kwa watumishi wengine ili kuendelea
kuboresha utendaji kazi na kuleta
mabadiliko chanya kwenye utekelezaji wa majukumu waliyonayo
Mafunzo hayo yaliyofanyika
katika Kampasi ya Mazumbai iliyoko Bumbuli mkoani Tanga yamewashirikisha
watumishi wote wa Kampasi hiyo ambayo SUA huitumia kwa tafiti mbalimbali za
misitu
0 Comments