SUAMEDIA

WATU ZAIDI MILLION 800 KUKUMBWA NA BAA LA NJAA ULIMWENGUNI IFIKAPO MWAKA 2030.

 Na.Vedasto George.

DUNIA inatarajiwa kuwa na upungufu mkubwa wa chakula ifikapo mwaka 2030 kutokana na athari za mabadiliko ya tabia nchi, ambapo hali hiyo itasababisha watu zaidi million 800 kukumbwa na baa la njaa, hivyo jitihada za ziada kwenye utafiti wa kilimo zinahitajika ili kukabiliana na hali hiyo.


Hayo yamebainishwa na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo SUA Prof. Maulid Mwatawala kulingana na ripoti ya shirika la chakula duniani ya mwaka 2020 Mjini Morogoro wakati akifungua kongamano la wadau wa kilimo ambalo linajadili masuala mbalimbali ya kuboresha kilimo ikolojia.


Naye Mkurugenzi Kurugenzi ya Mafunzo ya Uzamili,Utafiti, Uhaulishaji Teknolojia na Ushauri wa Kitaalamu kutoka SUA Prof. Esron Karimuribo amesema wametekeleza wito wa katibu mkuu wa umoja wa mataifa Antonio Gutteres juu ya kuwataka wadau wa chakula duniani kuandaa mijadala kama hii , ili kuboresha mifumo ya chakukla.



 




Post a Comment

0 Comments