SUAMEDIA

Waandishi wa Habari mkoani Morogoro watakiwa kuwa wazalendo

 

Na.Vedasto George

Waandishi wa habari mkoani Morogoro wamesisitizwa kuwa wazalendo na kufanya kazi kwa kufuata misingi,taratibu ya taaluma ya habari ikiwemo  kutanguliza masilahi  ya Taifa.





Msisitizo huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Bw. Bakari Msulwa katika Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari ambayo ufanyika kila ifikapo tarehe 3 mei na kusema kuwa kitu pekee ambacho kinaweza kumtambulisha muandishi wa habari katika jamii na Taifa ni jinsi anavyofanya kazi kwa kufuata misingi ya taaluma hiyo ubunifu na kutanguliza maslahi ya Taifa.

Msulwa ameongeza kuwa Serikali ya awamu ya sita itaendelea kuheshimu na kuthamini mchango mkubwa unaotolewa na vyombo vya habari nchini huku akibainisha kuwa Serikali pia itaendelea    kuweka mazingira mazuri ya ufanyaji kazi kwa wanahabari pamoja na upatikanaji wa habari zenye mlengo wa kujenga Taifa.

Aidha Msulwa amekitaka Chama cha Wahandishi wa Habari Mkoa wa Morogoro kuanzisha Miradi mbalimbali ya Maendeleo ambayo itawawezesha waandishi wa habari mkoani humo kuweza kujipatia kipato nje na kazi yao wa uandishi wa habari.

Kwa upande wao baadhi ya waandishi wa habari akiwemo Simon Mogela na Dastani Ibraimu wameiomba Serikali kuziangalia upya Sharia zinazoongoza Vyombo vya Habari ili kuweza kutoa  fursa kwa wanahabari kuweza kutekeleza majukumu yao kwa ufasaha.

Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari kote duniani uadhimishwa kila ifikapo Mei 3 kila mwaka ambapo Maadhimisho ya mwaka huu yalibebwa na kaulimbiu isemayo "HABARI KWA MANUFAA YA UMMA"

 

 

 

 

 

Post a Comment

0 Comments