SUAMEDIA

Wajasiriamali na Wasindikaji wa Vyakula Manispaa ya Morogoro wakishukuru Chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA kwa mafunzo ya usindikaji wa vyakula


Na.Ayoubu Mwigune

Wajasiriamali na Wasindikaji wa Vyakula mbalimbali kutoka Manispaa ya Morogoro wamekishukuru Chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA kwa mafunzo ya usindikaji wa vyakula.


  

Wakitoa maneno ya shukurani katika kuhitimisha mafunzo hayo ya siku mbili, Bi Esther Muffui, Joyce Edwin pamoja na Ramadhan Sigaleti  wamesema mafunzo hayo yamewanufaisha hasanamna ya  kupata nembo ya ubora kutoka katika shirika la viwango nchini tanzania TBS  jambo ambalo lilikuwa changamoto kubwa kwao

Wamesema kuwa  watakuwa  mabalozi wazuri kwa taaluma waliyojengewa na Chuo hicho wakibainisha  kuwa watazidisha ufanisi ili kuweza kulifikia soko la kimataifa


Kwa upande wake Bi. Nuria Majaliwa mhadhiri, Idara ya Teknolojia ya Chakula, Lishe  na Sayansi ya Mlaji ambaye pia alikuwa Mwezeshaji katika Semina hiyo amesema dhumuni la mafunzo hayo nikuwapa elimu na  kupanua wigo wao wa biashara ili kuzalisha bidhaa bora na salama huku akiwaomba kuyafanyia kazi yale yote ambayo wameweza kupata kupitia semina hiyo 

Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA  kimeandaa Semina kwaajili ya mafunzo kwa Wasindikaji wa vyakula mbalimbali kutoka manispaa ya Morogoro kwa  lengo la kuhakikisha kazi mbalimbali za kitafiti na kiteknolija  za Chuo hicho zinawafikia Watu mbalimbali katika Jamii mafunzo ambayo yamehitimishwa leo hii.






Post a Comment

0 Comments