SUAMEDIA

SUA kimewahahakishia wanafunzi watakaojiunga na chuo kuwa usajili wao kwa njia ya tehema ni wa uhakika

 

Na: Tatyana Celestine

Kituo cha TEHAMA katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA kimewahahakishia wanafunzi watakaojiunga na chuo hicho kuwa usajili wao kwa njia ya tehema ni wa uhakika maana wamejiandaa vyema kufanya kazi hiyo.




Akizungumza na SUA Media Mkurugenzi wa Kituo cha TEHAMA Dkt. Ayoub Churi amesema kuwa mawasiliano ya kimtandao yameimarishwa na mifumo yote imekaa vizuri ili kila anayetaka kusajili aweze kusajiliwa bila usumbufu wowote

Akizungumzia idadi ya wanafunzi wanaokuja kwa siku na jinsi ya wanavyokabiliana nao kwa udahili Dkt. Churi amesema kuwa chuo kimepeleka idadi ya kutosha ya wafanyakazi ili kurahisisha zoezi hilo linaloendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam


Ameongeza kuwa Kituo cha TEHAMA kimejiimarisha katika miundo mbinu ya kufundishia na kuwata wanafunzi wanaokidhi vigezo kujitokeza kwa wingi wakiwemo wale wanaotaka kujisomea kupitia njia mtandao


“Nawakaribisha kwasababu chuo chetu kimejihimarisha vizuri ikiwa ni pamoja na mtandao unaotosheleza kielimu, kupata kusoma vitabu na maabara zipo za kutoasha kwa ajili ya waafunzi ivyo tuna wakariisha sana sua” alisema Churi.

TC/                                                  MWISHO







Post a Comment

0 Comments