Na. Vedasto George
Naibu Waziri wa Maji Jumaa Aweso amesema changamoto kubwa inayo kwamisha wakulima nchini kuzalisha mazao yenye ubora wa hali ya juu ni ukosefu wa mbegu zenye sifa ambazo zinaweza kuwa na tija kwa wakulima na taifa.
Akizungumza mara baada ya kutembelea Maonesho ya 26 ya Wakulima maarufu Nanenane Kanda ya Mashariki yanayofanyika Mkoa wa Morogoro Aweso amesema kuwa ipo haja ya Wizara husika kuangalia kwa kina uwezekano wa upatikanaji wa mbegu bora zinazoweza kuwa mkombozi kwa wakulima nchini.
Aidha Aweso ameongeza kuwa wizara ya maji tayali imeishafanya mageuzi makubwa katika wizara hiyo ambapo wahandisi wa maji takribani 67 tayali wameisha futwa kazi kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao ipaswavyo.
0 Comments