SUAMEDIA

SUA KUZALISHA WATAALAMU WA KIWANGO CHA JUU ILI KUKABILIANA NA CHANGAMOTO YA KUTOWEKA KWA MISITU

Na Vedasto George na Gerald Lwomile

Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo SUA kupitia mradi wa “REFOREST” unaofadhiliwa na Serikali ya Sweden kwa kushirikiana na Shirika la maendeleo la SIDA kimeanzisha  kozi mpya ya Shahada ya Uzamivu ya  Sayansi za Misitu lengo likiwa ni kuzalisha wataalamu ambao watasaidia kutatua changamoto  zilizopo kwenye misitu katika ukanda wa Afrika.


Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Prof. Raphael Chibunda (katika waliokaa) akiwa na viongozi mbalimbali wa Chuo na wanafunzi wa kozi ya Uzamivu waliosimama, kulia waliokaa ni Mratibu wa kozi Prof. Romanus Ishengoma

 Akizungumza katika mafunzo na wiki ya kuwakaribisha wanafunzi 20 kutoka nchi tano za Tanzania, Rwanda, Uganda, Msumbiji na Ethiopia ambao wamechaguliwa kujiunga na kozi hiyo mpya katika chuo cha SUA Prof. Romanus Ishengoma amesema ili kuwafanya wanafunzi hao waweze kuwa mahiri katika masuala ya misitu watafanya tafiti mbalimbali zinazojikita katika misitu ili kuona ni namna gani wanaweza kuja na majibu ya changamoto zinazokabili misitu katika Afrika ikiwemo nchi zilizoko kusini mwa Jangwa la Sahara.

wanafunzi hawa Ili wote tuwalete kwenye uelewa unaofanana tutawafundisha darasani kwa mwaka mzima, pili wanafunzi hawa  watafanya utafiti kwenye nchi zao na kuandika tafiti zile kwa kipindi cha miaka mitatu, wakiwa kwenye Nchi zao watasimamiwa na walimu walioko kule kwenye kipindi cha masomo ya darasani  hawatafundishwa na walimu walioko SUA tu  tutachukua walimu pia kutoka kwenye vyuo vilivyo kwenye nchi zao maana yake ni nini  tunachukua ukanda wa Afrika Mashariki na kidogo Kusini ili kutengeneza progamu moja  ambayo wote  tunaunganisha nguvu”, amesema Pro.Romanusi Ishengoma.

Akizungumzia matarajio  na faidi zitakazotokana na kozi hiyo Prof. Ishengoma amesema  Chuo kitaweza kuzalisha wanafunzi ambao wataweza  kuondoa changamoto ya upotevu wa misitu katika hichi hizo tano  za  Afrika na kusisitiza  kuwa Chuo kitaweza  kushirikiana na wadau ili kuweza kuzalisha wataalamu ambao wataleta mchango mkubwa katika kuhifadhi misitu.

Kupotea kwa misitu ni tatizo kubwa  na ili uweze kulitatua tatizo hili  kiutaalamu ni pamoja na  kuwa na wataalamu wa kuweza kutatua haya  kwahiyo sisi tutafundisha watu ambao  watakuwa na upeo mkubwa  wa kuweza kusaidia kutatua haya matatizo makubwa ya misitu ambayo tunayaona misitu inapotea kila wakati, misitu inabadilishwa matumizi kuwa ya kilimo kwenye kipindi ambacho tunategemea misitu hii ichangie hasa katika suala zima la pato la Taifa” Amesema Prof. Pro.Romanus Ishengoma.

Kwa upande wake Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine Cha Kilimo (SUA) Prof.Raphael Chibunda amesema  uwepo wa Mradi wa “REFOREST” SUA umedhihirisha ubora wa Chuo hicho Barani Afrika na Duniani kwa ujumla

 Na uwepo wa huu mradi unaonesha ubora wa Chuo chetu ukilinganisha na vyuo vingine katika ukanda huu wa Africa lakini na Duniani kwa sababu Chuo chetu kilishindana  na vyuo vikuu vya nchi nyingine ili kupata nafasi ya kuwa mwenyeji wa program hii kwa sababu kuu ya miundombinu ya ufundishaji  katika maeneo ya misitu ambayo chuo kimejiwekea kwa kipindi cha muda mrefu tukaweza kushinda na kupewa nafasi hii” , amesema Prof. Chibunda.

Aidha Prof. Chibunda ameongeza kuwa SUA ndiyo Chuo Kikuu peke yake katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika  ambacho kinafundisha misitu na kuweza kumiliki misitu ambayo inatumika kufundishia na kuweza kuzalisha mazao mbalimbali yatokanayo na misitu.

“Sisi tuna eneo kubwa la misitu katika mkoa wa Arusha pale Olomotonyi ambapo tuna zaidi ya hekta 800 za kupandwa lakini  pia katika mkoa wa Tanga kwenye milima ya usambaa eneo la Mazumbai tuna msitu wa asili karibu hekta 320, vilevile tumefungua shamba jipya la msitu lenye ukubwa wa hekta 10,000 msitu wa biashara katika mkoa wa Ruvuma” Amesema Prof Chibunda.

Zaidi ya Wanafunzi 300 kutoka mataifa mbalimbali waliomba kusoma kozi hiyo ya Shahada ya Uzamivu ya  Sayansi za Misitu ambapo wanafunzi 20 tu ndiyo waliofuzu na kuwa na vigezo huku watano wakiwa ni kutoka katika nchi ya  Tanzania, watatu kutoka nchini Msumbiji, wanne kutoka nchi ya Rwanda, wanne kutoka Uganda, na  wengine wanne ni kutoka Ethiopia kati yao asilimia 45 wakiwa ni  wasichana.

Post a Comment

0 Comments