SUAMEDIA

SUA KUHAKIKISHA UVUMBUZI NA UBUNIFU WA WANAFUNZI UNAKUWA NA HATI MILIKI

 

Na Gerald Lwomile

Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimewahakikishia wanafunzi wote wanaosoma chuoni hapo katika Shahada za Juu kuwa kimeweka mazingira mazuri ya kuhakikisha umiliki wa uvumbuzi na ubunifu unaofanywa na wanafunzi hao unalindwa kisheria

Akizungumza leo Januari 29, 2021 katika Siku ya Kuyajua Mazingira ya SUA kwa wanafunzi wanaosoma Shahada za Umahili na Uzamivu, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine upande wa Taaluma Prof. Maulid Mwatawala amesema hiyo itasaidia mwanafunzi kumiliki kisheria uvumbuzi na ubunifu wake


Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine upande wa Taaluma Prof. Maulid Mwatawala akisisitiza kuhusu jambo wakati akifungua Siku ya Kuyajua Mazingira ya SUA kwa wanafunzi (hawapo pichani) Picha na Vedasto George

“Tumeanzisha kitengo maalumu ili kuhakikisha  uvumbuzi na ubunifu unaofanywa na wanafunzi waliofanya tafiti katika SUA unalindwa kisheria” amesema Prof. Mwatawala

Akizungumzia kwa upande wa muda wa masomo Prof. Mwatawala amewataka wanafunzi hao kuhakikisha wanautumia vizuri muda wao kwa kusoma kwa bidii na kufanya tafiti ili kuwa miongoni mwa Majalisi wa Chuo hicho

Awali akimkaribisha Mgeni Rasmi ili kufungua Siku hiyo ya Kuyajua Mazingira ya SUA Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Uzamili, Utafiti, Uhaulishaji wa Teknolojia na Ushauri wa Kitalaamu Prof. Erson Karimuribo amesema katika siku za hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la wanafunzi wanajiunga na Shahada za Juu chuoni hapo na hii ni ishara kuwa Chuo kinatoa wahitimu bora

Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Uzamili, Utafiti, Uhaulishaji wa Teknolojia na Ushauri wa Kitalaamu Prof. Erson Karimuribo akizungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi 

Amesema kwa mwaka huu kumekuwa na ongezeko kubwa tangia kuwepo kwa wanafunzi 176 mwaka 2016 hadi kufikia wanafunzi zaidi ya 240 mwaka huu

“Tuna kila sababu ya kulishukuru Baraza la Chuo na  Menejimenti kwa ujumla kwa kutupa ushirikiano mkubwa uliowezesha kuwepo kwa ongezeko la wanafunzi na kwa kweli hakuna shaka kabisa baada ya ongezeko kutoka wanafunzi 176 mwaka 2016 hadi kufikia wanafunzi 240 mwaka 2021” amesema Prof Karimuribo

Naye Mratibu wa Masomo ya Shahada za Umahili na Uzamivu katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA Dk. Akwilina Mwanri akitoa neno la shukrani kwa mgeni Rasmi amesema anayo matumaini makubwa kuwa wanafunzi waliojinga na Shahada hizo watamaliza Chuo kwa wakati na kuwa Majarisi wa Chuo hicho


Mratibu wa Masomo ya Shahada za Umahili na Uzamivu katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA Dk. Akwilina Mwanri akitoa neno la shukrani

Dk. Mwanri ameongeza kuwa ni muhimu kwa wanafunzi hao kuhakikisha wanafanya vizuri kwa kusoma kwa bidii na Chuo kitatoa ushirikiano wa kutosha kwa wanafunzi wote

Baadhi ya wanafunzi wa Shahada za Juu wakisikiliza hotuba ya Mgeni Rasmi (hayupo pichani) wakati wa Siku ya Kuyajua Mazingira ya SUA


Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine upande wa Taaluma Prof. Maulid Mwatawala aliyevaa tai nyekundu mbele akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na wanafunzi wa Shahada za juu


Post a Comment

0 Comments