SUAMEDIA

Ufugaji wa kuku una mchango katika kuondoa umaskini

 Na: Vumilia Kondo

Mafunzo ya ufugaji bora wa kuku kwa wafugaji 23 kutoka mikoa mbalimbali nchini, yamemalizika Novemba 20  katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA, yakilenga kuongeza uzalishaji wa mayai na nyama pamoja na kuboresha lishe ya jamii.

Afisa Tawala wilaya ya Morogoro Bw.
Hilary Sagala waliokaa (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wakulina na wataalamu. wa pili kutoka (kushoto) ni Rasi wa Ndaki ya Misitu, Wanyamapori na Utalii Prof. Agnes Sirima

Akifunga mafunzo hayo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Hilary Sagala ambaye ni Afisa Tawala  amesema ufugaji bora wa kuku una mchango mkubwa katika kupunguza umasikini

Amesema watumishi wengi na wafanyakazi wa sekta binafsi wanapaswa kupata nafasi ya kujifunza ili hata wanapostaafu waweze kuwa na shughuli za kukuza uchumi wao na kupunguza umaskini katika Kaya.


Kwa upande wake, mwakilishi wa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo ambaye ni Rasi wa Ndaki ya Misitu, Wanyamapori na Utalii Prof. Agnes Sirima amesema SUA itaendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali ili kuhakikisha elimu ya kitaalamu inawafikia wafugaji zaidi nchini.

Naye mwakilishi wa Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Kujiendeleza ICE Dkt. Emmanuel Malisa amesema mafunzo hayo yaliyodumu kwa siku nne yamehusisha nadharia na vitendo, ikiwemo ulishaji wa vifaranga, ujenzi wa mabanda, chanjo na mbinu za biashara.



Kwa upande wake Profea Tiisekwa Bendantungukwa kutoka AICAD amesema ufugaji wa kuku ni eneo linaloweza kuleta matokeo ya haraka, hivyo elimu hiyo inawajengea uwezo washiriki kuongeza kipato na usalama wa chakula majumbani.

Baadhi ya washiriki wamesema mafunzo hayo yamewasaidia kuelewa namna ya kupunguza vifo vya kuku na kupata tija zaidi katika uzalishaji.


Post a Comment

0 Comments