SUAMEDIA

SUA yawapa elimu na pongezi wanafunzi wa mwaka kwanza 2025/2026

 Na: Ngolo Mboje

Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali ikiwemo Ofisi ya Uhamiaji mkoani Morogoro, kimetoa elimu na kuwapongeza wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliojiunga na chuo hicho kwa mwaka wa masomo 2025/2026.


Akizungumza katika mkutano uliofanyika katika Kampasi ya Edward Moringe Sokoine, November 17 2025 Kaimu Mkuu wa  Kitengo Cha Mawasiliano na Masoko wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha kilimo ( SUA) Bi. Suzan Magobeko, amewaapongeza wanafunzi hao na kuwataka kuwa mabalozi wazuri wa chuo, hususan kupitia mitandao ya kijamii.

Aidha, Kaimu Mkuu Mlezi wa Idara ya Ushauri kwa Wanafunzi SUA, Bi. Hilda Gamuya, amesema kuwa mwitikio wa wanafunzi wa mwaka huu ni mzuri tofauti na mwaka wa masomo 2024/2025, kwani wana imani kuwa elimu wanayoitoa inaweza kuleta hamasa na mtazamo chanya ili kuendana na utaratibu wa chuo.

Bi. Hilda ameongeza kuwa matarajio yao makubwa ni kuona wanafunzi wanabadilika na kuendana na utaratibu, sheria na kanuni za chuo, lengo likiwa ni kuwajengea misingi bora ya maisha wawapo katika kampasi chuoni hapo.


Kwa upande wake, Afisa Usajili wa Mkoa wa Morogoro, Bw. James Malimo, ameeleza umuhimu wa wanafunzi kuwa na namba ya NIDA, akisema kuwa namba hiyo itawasaidia kupata huduma mbalimbali ikiwemo huduma za afya, mikopo, pamoja na kuepusha usumbufu wa kukosa huduma muhimu kwa wakati.pia itawasaidia kutambulika

Aidha, Bw. James ametoa wito Kwa wanafunzi hao kutoa taarifa sahihi wakati wa mchakato wa usajili, kwani taarifa hizo zitawasaidia katika masuala ya elimu na maisha yao kwa ujumla.na kuwataka wajitokeze kwa wingi kujisajili.

Nao wanafunzi wa mwaka wa kwanza, Bi. Laisa Bakari na Robert Laurent, walieleza namna walivyopokelewa chuoni hapo, wakisema mapokezi yao yamekuwa mazuri na kwamba elimu waliyopewa itawasaidia kufuata sheria, kanuni na utaratibu wa chuo. Aidha, wamesema matarajio yao ni kuanza masomo yao rasmi kwa mafanikio.




Post a Comment

0 Comments