Na: Gerald Lwomile
Imeelezwa kuwa kutokana na
umuhimu wa zao la mpunga kibiashara na chakula, uzalishaji wake umeambatana na
matumizi holela ya mbolea hasa aina ya naitrogen ambapo kiasi kinachozidi
huchangia uchafuzi wa maii na kuongeza gesi chafuzi aina ya nitrous oxide
kwenye anga la dunia.
| Profesa Mshiriki na Kaimu Mratibu wa Masomo ya Umahiri na Uzamivu Prof. Akwilina Mwanri wa pili kutoka kulia mstali wa mbele akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Mradi wa SUNIRICE |
Prof. Akwilina amesema utafiti utakaofanywa na mradi huo utasaidia kupunguza matumizi holela ya mbolea ili kuthibiti kiwango cha ges chafusi na kuwa kilimo endelevu cha mpunga..
Amesema Chuo Kikuu cha Sokoine
cha Kilimo kitahakikisha kinatoa ushirikiano wa kutosha kuhakikisha utafiti huo
unafanyika na kuleta matokeo.
“Nimefurahi sana kuona RECODA
wapo katika mradi huu kwani kuna wakati tunafanya tafiti nyingi lakini
tunashindwa kuzifikisha kwa wanufaika na badala yake tunaishia kwenye
makabrasha na kutoa machapisho tu” amesema” Prof. Mwanri
Akitoa ufafanuzi namna mradi
utakavyofanya kazi Kiongozi wa Mradi huo Dkt. Beatrice Mwaipopo amesema mradi
utajikita katika kuangalia namna wakulima wa mpunga wanavyoweza kutumia mbolea
zenye Nitrojeni kuzalisha mpunga na kuepusha madhara yake kwa kutumia mbolea
ipasavyo.
| Kiongozi wa Mradi huo Dkt. Beatrice Mwaipopo akifafanua kuhusu Mradi wa SANIRICE |
Mradi huo unashirikisha Chuo
Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, na Wakala wa mbolea TFRA, na asasi isiyo ya
kiserikali inayojihusisha na usambazaji wa teknolojia kwa wakulima, RECODA.
0 Comments