Na: Calvin Gwabara - Dara ess salaam
Mwenyeji mwenza wa mkutano huo, Prof. Joyce Kinabo kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), ametoa wito wa kuendeleza ushirikiano, utekelezaji wa sera zinazotegemea ushahidi wa kisayansi, na ubunifu wa kisekta ili kukabiliana na changamoto za kimataifa katika mifumo ya chakula na afya ya umma.
![]() |
Mwenyeji mwenza wa mkutano huo, Prof. Joyce Kinabo kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) akito hotuba ya kufunga Mkutano huo wa kimataifa jijini Dar es salaam. |
Prof.
Kinabo alishukuru Chuo Kikuu cha London cha Usafi wa Mazingira na Tiba ya
Kitropiki (LSHTM) kwa kuchagua Tanzania na Chuo Kikuu cha Sokoine kuwa wenyeji
wa tukio hili kubwa la kimataifa na kueleza fursa hiyo kuwa ni heshima kubwa na
ishara ya kutambua mchango wa Tanzania katika kuunda sera za kimataifa kuhusu
chakula na afya.
“Tuendelee
kutumia maarifa na uhusiano tulioupata hapa katika kazi zetu na ushirikiano wa
baadaye,” Alisema Prof. Kinabo.
Aidha
alieleza kwa muhtasari mambo muhimu yaliyoibuliwa katika mkutano huo,
akisisitiza umuhimu wa mawasiliano baina ya sekta na taaluma mbalimbali,
mshikamano kati ya utafiti na sera, na uhitaji wa kuwekeza zaidi katika mifumo
ya maarifa hata hivyo alionya kuhusu hatari zinazoongezeka kama vile ulaji wa
vyakula vilivyosindikwa kupita kiasi (UPFs), matumizi ya plastiki, na sumu
katika chakula, ambavyo vinachukua nafasi ya lishe bora katika jamii nyingi.
Akitoa
wito wa hatua za kuchukua alisisitiza kuwa changamoto tata zilizojadiliwa
katika mkutano huu haziwezi kutatuliwa kwa njia za kisekta pekee bali aliwataka
washiriki kutafsiri elimu waliyopata kuwa vitendo, kuendeleza ushirikiano baina
ya mataifa na fani mbalimbali, na kuleta mabadiliko ya kimfumo.
“Sasa na baadaye viko mikononi mwetu,” alisema
Prof. Kinabo.
Prof.
Kinabo pia alitoa shukrani kwa wawasilishaji wa mada, watafiti, washirika wa
utekelezaji, na wafadhili waliofanikisha mkutano huo, na kumalizia kwa kuwataka
washiriki kutazama mbele, akihimiza utafiti zaidi, uundaji wa vipimo vya pamoja
vya kutathmini programu, na utekelezaji wa sera zinazotegemea ushahidi.
“Huu
si mwisho, bali ni mwanzo wa fursa mpya na ushirikiano mpana zaidi,” alisema,
kabla ya kutangaza rasmi kufungwa kwa mkutano wa kitaaluma wa ANH2025.
![]() |
Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma Utafiti na ushauri wa Kitaalamu Prof. Maulid Mwatawala akizungumza kwenye kama mmoja wa wachokoza mada. |
0 Comments