Na: Calvin Gwabara - Arusha.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Johari amefuturisha
Mawakili wa Serikali kutoka taasisi mbalimbali za Serikali nchini wanaoshiriki
mafunzo ya pili ya mwaka ya Mawakili wa Serikali nchini Jijini Arusha.
Hafla hiyo imeongozwa na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Samwel M. Maneno na Mwandishi Mkuu wa Sheria nchini Bwana Onorius Njole.
![]() |
1. Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Samwel M. Maneno (wa kwanza kushoto) na Mwandishi Mkuu wa Sheria nchini Bwana Onorius Njole (kulia) wakiongoza Mawakili wa serikali kupata Iftar.
PICHA ZA MATUKIO YA
IFTARI ILIYOFANYIKA KWENYE HOTEL YA MAUNT MERU JIJINI ARUSHA.
![]() |
1. Mwandishi Mkuu wa Sheria nchini Bwana Onorius Njole (katikati mwenye nguo nyeusi) akiwa kwenye picha na wafanyakazi wa ofisi yake mara baada ya kumaliza Iftar.
![]() |
1. Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Samwel M. Maneno (kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Uratibu na Huduma za Ushauri wa Kisheria wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bi Neema Ringo.
![]() |
1. Mwandishi Mkuu wa Sheria nchini Bwana Onorius Njole (katikati mwenye nguo nyeusi) akiwa kwenye picha na wafanyakazi wa ofisi yake mara baada ya kumaliza Iftar.
![]() |
1. Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Samwel M. Maneno (kulia) akiteta jambo na Mwandishi Mkuu wa Sheria nchini Bwana Onorius Njole (wa kwanza kushoto) wakati wa iftar.
0 Comments