SUAMEDIA

Wakulima wameaswa kutembelea Banda la SUA katika Idara ya Sayansi ya Udongo na Jiolojia ili kupima Sampuli za Udongo kwa Kilimo chenye Tija

 NA:Winfrida Nicolaus

Wakulima pamoja na watu wanaohitaji kuingia katika shughuli za Kilimo wametakiwa kutembelea banda la SUA katika Idara ya Sayansi ya Udongo na Jiolojia kwenye Maonesho ya 29 yaWakulima, Wafugaji na Wavuvi kanda ya Mashariki yanayofanyika mkoani Morogoro ili kupima Sampuli zao za Udongo kwaajili ya Kilimo chenye Tija na Endelevu.

Mtaalam wa Udongo Bw. Louis Mdoe kutoka Ndaki ya Kilimo, Idara ya Sayansi ya Udongo na Jiolojia katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA wakati akizungumza kuhusu umuhimu wa kupima udongo kabla ya kuanza kulima.

Amesema hayo Mtaalam wa Udongo Bw. Louis Mdoe kutoka Ndaki ya Kilimo, Idara ya Sayansi ya Udongo na Jiolojia katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA wakati akizungumza Mubashara na SUA FM kutoka kwenye viwanja vya Maonesho hayo.

Amesema kuna umuhimu mkubwa kwa Wakulima kujua vipimo vya Udongo kwa kuwa vinawasaidia kutambua aina ya zao kwenye Udongo husika vilevile aina ya Virutubisho katika shamba lake kwa mazao husika na kwamba hiyo inapelekea mkulima kuwa na kilimo cha uhakika na cha tija.

Bw. Mdoe amesema kuna Virutubisho kama Salfa, Nitrojeni, Potasium, Calsium pamoja na Magnesium yapo baadhi ya mazao ambayo yanapendelea hivyo Virutubisho hivyo unapokuwa umepima Udongo wako unaweza ukajua ni aina gani ya zao unaweza ukalipanda katika shamba lako ili kujipatia Tija kwenye mavuno yako.

“Umuhimu wa kujua Vipimo vya Udongo vinakusaidia katika kujua ni zao  gani ulime kwasababu baadhi ya mazao yanahitaji aina Fulani ya Udongo na baadhi ya mazao yanahitaji aina fulani ya Virutubisho kwa wingi kwa hiyo unapojua shamba lako lina virutubisho vya aina gani itakusaidia kujua zao gani linapenda virutubisho vya aina hiyo vilevile aina ya udongo kwa zao fulani ”, amesema Mdoe.

“Kwa mfano ukachukua sampuli ya udongo wako halafu ukajua udongo wako huo una kiasi kikubwa cha mfinyanzi na tunafahamu kuwa udongo huo wa mfinyanzi unatabia ya kukwamisha maji kwa kiasi kikubwa kwa hiyo ni vizuri ukachagua zao ambalo linahitaji eneo la kutuamisha maji ambalo ni Mpunga”, amesema Mdoe.

Aidha amesema kama Mkulima anahitaji kuchukua Sampuli ya Udongo katika shamba lake ni muhimu kumtumia Mtaalam ambaye anaweza kuchukua sampuli hiyo kitaalam kwasababu sampuli yoyote ile ya udongo inauwakilishi kulingani na ukubwa wa eneo la shamba lako.

“Kwa mfano sampuli ya Udongo inayowakilisha kiasi cha Tani 20,000 kwa Ekali Moja katika Tani hizo 20,000 unaweza ukaleta Udongo wa Kilo Moja na ndio uwakilishi husika kwa hiyo unatakiwa uchukue sampuli yako kama una Elimu ya Sayansi ya Kilimo na si mtu yoyote yule kwasababu anaweza kuleta Sampuli ambayo si wakilishi kwa eneo husika”, amesema Mtaalam huyo.





 

 

Post a Comment

0 Comments