Na: Gojo Mohamed
Wanafunzi wa Shahada ya Kwanza katika Kozi ya Utalii Mapumziko Uishi kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) wametengeneza njia ya watembea kwa miguu kwa ajili ya watalii pamoja na kutambua maeneo tofauti ya kupumzikia maarufu kama Camp Site katika bustani ya miti na maua yanayomilikiwa na SUA katika eneo la Morning Site Manispaa ya Morogoro.
![]() |
| PICHA NA MTANDAO |
Mhadhiri
kutoka Idara ya Utalii na Mapumziko Uishi SUA aliyekuwa akisimamia na kuratibu
shughuli hizo Bw. Semi Thadeo Mokiti amesema kuwa mambo makubwa ambayo
wanahusika nayo ni kuwaandaa vijana kuweza kuja kuwa wabunifu, wasimamizi na
waongozaji wa masuala ya utalii
Amesema
wanafunzi hao wa mwaka wa kwanza na baadhi yao
kutoka mwaka wa pili na wa tatu wamechukua hatua ya kuyatambua na
kutengeneza maeneo ya kupumzikia karibu na lango kuu la kuingia SUA ili kufufua
maeneo hayo kwa ajili ya shughuli za kiutalii chuoni hapo.
‘‘Kwa Mwaka huu wa
2022 katika mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wetu tumekuwa na programu maalumu
na hii ni moja ya harakati ya kumuunga mkono Rais wetu Mhe. Samia Suluhu Hassan
kuendeleza utalii katika nchi yetu na tulianza na kutengeneza njia kwa ajili ya
watalii kupita katika bustani ya ‘Bortanical Garden’ iliopo karibu na lango kuu la kuingia
SUA na kazi nyingine ni kuliendeleza eneo la Morning Site ’’. Amesema Mokiti
Ameongeza
kuwa licha ya wanafunzi kutengeneza njia kwa ajili ya watalii wanaofika SUA pia
wamefanikiwa kuanzisha camp site tatu mpya ambazo ni rasmi na za kuvutia kwa
ajili ya watu kupumzika
Kwa
upande wake Mwanafunzi Gudluck Tukai amesema kuwa amejifunza vitu vingi akiwa
darasani na hata nje ya darasa ambapo amejifunza na kufanya kwa vitendo hivyo
amewashauri wanafunzi wenzake katika kozi hiyo kufanya mazingira yawe yanavyotakiwa
Naye
Neema Lazaro amesema kupitia kazi walioifanya ya kufufua maeneo kwa ajili ya
utalii amejifunza namna ya kuandaa mazingira ambayo yatawafanya watalii waweze
kuvutiwa zaidi kutembelea maeneo ya utalii ikiwemo SUA Chuo ambacho kinatoa
mafunzo kwa nadharia pamoja na vitendo
.jpg)
0 Comments