SUAMEDIA

SUA kuendelea kufanya tafiti Mradi unaolenga kuzalisha Mbegu vumilivu ya Mpunga kwa Mabadiliko ya Tabia Nchi

Na,Winfrida Nicolaus

Wanafunzi wa Shahada ya Uzamili pamoja na wanafunzi wa Shahada ya Uzamivu kutoka kitengo cha Sayansi ya Mimea Ndani ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) wameendelea kufanya tafiti kwenye mradi unaolenga  kuzalisha Mbegu Vumilivu ya Mpunga kwa Mabadiliko ya Tabia Nchi (CLIMATE-SMART AFRICAN RICE) huku lengo likiwa ni kuwajengea uwezo na kuleta majibu ya tafiti zenye tija kwa maendeleo ya nchi

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania TARI Dkt. Atugonza Bilaro wakati wa mkutano wa siku tatu uliofanyika SUA naa kuendeshwa na washiriki toka Chuo Kikuu cha Copenhagen kilichopo nchini Denmark, Taasisi ya Utafiti wa Mpunga IRRI, Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania TARI pamoja na SUA ambao ndio wasimamizi wakuu wa mradi huo.

Dkt. Bilaro amesema kuwa ili kufikia uzalishaji wa mpunga wenye tija ni mchakato na wao kama wataalam wameona ni bora zaidi kuwatumia wanafunzi kwa kuwa watafanya kwa vitendo hatua kwa hatua hadi kufikia lengo la mradi huo la kuzalisha mbegu ya mpunga yenye tija na stahimilivu kwa mabadiliko ya tabia nchi

Amesema kupata watafiti wazuri kunahitaji jitihada za kutosha na jitihada hizo zipo katika kuwaandaa wanafunzi hao mapema kwa kuwashirikisha katika miradi mbalimbali katika kile wanachosomea ili waweze kuwa bora na hata kuaminiwa kutokana na uzoefu walionao.

‘‘Kwa hiyo nataka tu kusema wanafunzi hawa tunaowatumia katika mradi huu ndio hao watakuja hata katika mashirika yetu kwaajili ya kufanya kazi ingawa wengine ni wafanya kazi tayari hivyo basi watatusaidia kufanya kazi zenya tija na kuleta maendeleo kwa taifa kwasababu kwanza kabisa tunataka kufanya zao la mpunga kuwa la kibiashara hivyo bas mpaka kukamilika kwa mradi huu ambao utaendeshwa kwa muda wa miaka mitano ambao utawafanya kuwa bora zaidi’’. Amesema Dkt. Bilaro

Kwa upande wake Afisa Kiungo kati ya Serikali ya Tanzania na Shirika la Kimataifa la Utafiti wa Mpunga IRRI Bwana George Iranga amesema ushirikiano wa shirika la kitaifa la Utafiti wa Mpunga IRRI pamoja na SUA umeleta mafanikio mazuri sana katika sekta ya kilimo hivyo hatua iyo ya kushirikisha wanafunzi toka chuoni hapo katika mradi kutaleta ongezeko la watafiti wazuri na wenye uzoefu katika kutatua changamoto za wakulima nchini.

‘‘tupo hapa kama washirika ambao tumeshirikiana na Chuo Cha Sokoine Cha Kilimo SUA katika mradi huu ambao mpaka sasa una miaka miwili na unasehemu ya kuwafundisha wanafunzi katika levo ya uzamili, uzamivu Pamoja na kutoa kozi fupi katika kuwajengea uwezo ili waweze kutatua changamoto za wakulima hasa katika changamoto hii ya mabadiliko ya hali ya hewa kwa kuleta mbegu stahimilivu kwa kila mabadiliko ya tabia nchi na zenye tija’’. Amesema Bwana George Iranga








Post a Comment

0 Comments