SUAMEDIA

SUA, Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Shirika la ICARS la Denmark kufanya utafiti kupunguza matumizi ya madawa kwa kuku

 

Gerald Lwomile

Dodoma

Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Shirika la ‘International Centre for Antimicrobial Resistance Solutions’ (ICARS) la Denmark wameingia makubaliano ya kufanya utafiti wa kutumia chanjo na usafi katika kuthibiti magonjwa ya kuku nchini ili kupunguza matumizi ya dawa hususani dawa za antibiotiki ili kulinda afya za walaji.


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulege kushoto akimakaribisha  Prof. Robinson Mdegela ofisini kwake Jiji Dodoma

Akizungumza mara baada ya kupokea taarifa ya namna miradi miwili ya utafiti utakavyofanyika hapa nchini, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulege amesema kama utafiti huo utafanyika vizuri utaleta matokeo chanya kwa wafugaji ambao watatumia usafi na chanjo na kupunguza matumizi ya dawa kwenye kuku.

Awali akizungumza wakati akitoa taarifa ya miradi hiyo Mtafiti Kiongozi na Mhadhiri Mwandamizi kutoka SUA Prof. Robinson Mdegela amesema SUA na Wizara Mifugo na Uvuvi wameandika miradi miwili ya utafiti ambayo ni uwezekano wa kutumia njia za usafi kwenye mabanda ya kuku na  kuchanja kuku ili kudhibiti magonjwa ya kuku hivyo kupunguza matumizi ya madawa yasiyo ya lazima.


Mkurugenzi wa Uendeshaji wa ICARS Bibi. Helle Engslund Krarup kushoto akisaini makubalino ya kuanza kwa miradi hiyo, kulia ni Prof. Mdegela kutoa SUA

Prof. Mdegela amesema matumizi hayo yamesababisha vifo vingi duniani kote na inakadiriwa hadi kufikia mwaka 2050 zaidi ya watu milioni kumi wako hatarini kufa kutokana na matumizi ya mazao ya kuku kwa kula mabaki ya dawa ambayo madhara yake ni pamoja na usugu wa vimelea kwenye dawa.

“……, tunayo furaha kuwa shirika hili la ICARS la Denmark limekubali kufadhili miradi hii miwili kwani ukweli ni kuwa upo ushahidi matumizi ya mabaki ya dawa yanaleta madhara pamoja na usugu wa vimelea jambo linalohatarisha Maisha ya walaji” Amesema Prof. Mdegela

Naye Mkurugenzi wa Uendeshaji wa ICARS Bibi. Helle Engslund Krarup amesema na ukweli usio na shaka kuwa matumizi ya antibiotiki zitokanaza  na mabaki ya dawa kwenye mazao ya kuku ni tatizo kubwa duniani kote ambapo hadi kufikia mwaka 2019 zaidi ya watu milioni 5 walikufa huku nchi zilizoko Kusini mwa Afika zikipoteza zaidi ya watu laki mbili na elfu hamsini

“Serikali ya Denmark ikaona ni vyema Shirika hili la ICARS lifanye kazi na washirika wake ili kupata suluhisho la namna gani hali hii inaweza kudhibitiwa na kuwa tunayofuraha kufanya kazi na Wizara ya Mifugo na Uvuvi na SUA” amesema Bibi. Krarup

Post a Comment

0 Comments