SUAMEDIA

Wizara ya Elimu yaikabidhi SUA Vifaa vipya vyenye thamani ya zaidi ya Euro elfu 83 sawa na zaidi ya sh. Million 224.4

 Idara mpya ya Uhandisi Ujenzi na Rasilimali za Maji  ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA imepokea vifaa vipya vyenye thamani ya zaidi ya Euro elfu 83 ambazo ni sawa na zaidi ya sh. Million 224.4 kutoka serikalini kupitia Wizara ya Elimu ambavyo vitasaidia kuongeza ufanisi.

Mtekinolojia mwandamizi kutoka katika ya Idara ya Uhandisi Ujenzi na Rasilimali za Maji   Dkt Paul Reuben akielezea namna kifaa kinachotumika kupima tabia ya udongo kutokana na mgandamizo ili kujua uwezo wa udongo kustahimili mzigo juu yake kama majengo nk  (Triaxial Machine) kinavyofanya kazi.

 Mteknolojia Mwandamizi kutoka Idara hiyo Dkt. Paul Reuben amesema  ujio wa vifaa hivyo utaongeza ufanisi wa utendaji kazi  katika ufundishaji, utafiti,usimamizi wa miradi ya maendeleo kwa sekta za serikali na mashirika binafsi pamoja na ushauri wa kitaalamu.

‘’Tunaishukuru sana Serikali inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa

kutoa kipaumbele kwenye mafunzo kwa vitendo, hii itafanya wahitimu wawe na

ujuzi na maarifa hivyo kuweza kujiajiri wenyewe wanapokuwa wamemaliza

masomo yao”,alisema Dkt Reuben.


Dkt. Reuben amesema upatikanaji wa vifaa hivyo ni mwanzo wa kuimarisha Idara ambayo itatakiwa kuwa na maabara nyingine ili kuwezesha kufanyika kazi zote za vipimo vya vifaa vya ujenzi ndani ya maabara na sehemu mbalimbali ambako  ujenzi unafanyika.

‘’Awali wanafunzi iliwalazimu kusafiri kwenda Vyuo vingine kama vile Chuo Kikuu

cha Dar es salaam (UDSM) kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo huku masomo

mengine ikiwalazimu kufanya kwa nadharia zaidi kuliko vitendo”, ameeleza Dr.

Reuben.

Pamoja na shughuli nyingine vifaa hivyo vitatumika kuchunguza maeneo ambayo udongo wake unafaa kwaajili ya ujenzi wa mabwawa, mifereji ya umwagiliaji, ujenzi wa barabara pamoja na majengo.

Mteknolojia huyo amesema vifaa hivyo pia vitasaidia wahitimu kupata ajira kwa urahisi pindi wanapohitimu masomo yao.



Kifaa kinachotumika kupima tabia ya udongo kutokana na mgandamizo ili kujua uwezo wa udongo kustahimili mzigo juu yake kama majengo nk  (Triaxial Machine).

Mtekinolojia mwandamizi kutoka katika ya Idara ya Uhandisi Ujenzi na Rasilimali za Maji   Dkt Paul Reuben akielezea namna kifaa cha kukaushia sampuli za udongo majani nakadhalika (Drying Oven) kinavyofanya kazi.


Kifaa cha kupimia vitu vyenye uzito mdogo mpaka gram 210 (Weighing Balance).


Kifaa cha kupima ubora wa matofali na zege kwa ajili ya ujenzi (Compression Machine).



Post a Comment

0 Comments