SUAMEDIA

Kuelekea Miaka 60 ya Uhuru SUA inatambua mchango wa wakulima kuhakikisha Usalama wa Chakula


Na Gerald Lwomile

Mwanza

Katika kuadhimisha Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere na Chuo Kikuu cha Mt. Augustine (SAUT) tarehe 01 Desemba, 2021 kinatarajia kufanya Kongamano la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara katika Chuo Kikuu cha SAUT Jijini Mwanza


Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Prof. Raphael Chibunda akimuonyesha  teknolojia mbalimbali  Dk. Dolphine Kessy Mhadhiri SAUT aliyevaa miwani katikati

Akizungumza leo Novemba 30, 2021 katika mkutano wake na waandishi wa habari Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Prof. Raphael Chibunda amesema Kongamano hilo litajadili mada mbalimbali ikiwemo maendeleo ya kilimo nchini

Prof. Chibunda amesema katika miaka 60 ya Uhuru wakulima wa Tanzania wamefanya kazi kubwa katika kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika uzalishaji wa mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi na hivyo kupelekea taifa kukabiliana na upungufu wa chakula unapojitokeza


Prof. Chibunda katikati waliokaa mbele akizungumza wa waandishi wa habari kulia kwake ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma, Utafit na Ushauri wa Kitaalamu Prof. Maulid Mwatawala

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo ameendelea kusema kuwa uzalishaji bora wa nyama unaofanywa na wafugaji nchini pia umesaidia kuwepo kwa nyama wakati wote

Akizungumzia suala la uvuvi Prof. Chibunda amesema watafiti nchini wakiwemo wale wa SUA wameendelea kuhakikisha wanakabiliana na magonjwa ya Samaki lakini pia kuongeza uzalishaji wa Samaki kwa kuzalisha vifaranga bora na kuinua lishe na pato la mwananchi

Prof. Chibunda amesema katika kuhakikisha kongamano hilo linajadili kwa undani maendeleo ya kilimo nchini wamechagua kauli mbiu isemayo “Mchango wa Sekta ya Kilimo Katika Maendeleo ya Tanzania: Mafanikio na Changamato Baada ya Miaka 60 ya Uhuru”.

Aidha SUA katika kuitikia wito wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeanza maonesho katika Chuo cha SAUT ambapo inaonesha teknolojia na ubunifu mbalimbali unaofanyika SUA.

KATIKA VIDEO



Post a Comment

0 Comments