Na.Vedasto George.
Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA kimeendelea na jitihada
zake za kuunga mkono sera za nchi na
mwelekeo wa taifa kuelekea kukuza uchumi wa viwanda kwa kuhakikisha kinatoa wataalam wenye ujuzi na maarifa
ambayo yatasaidia katika kuinua uchumi wa viwanda vidogo na vya kati ambavyo
vimenzishwa nchini.
![]() |
Mratibu wa Utafiti na Machapisho SUA Prof. Japhet Kashaigili akifungua Mafunzo ya Kongano la Nguo mjini Morogoro yaliyoratibiwa na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA Morogoro. |
"Kituo cha
Ubunifu kilichopo katika Kurugenzi hii kimejikita katika kutoa elimu ya
bunifu mbalimbali, hati miliki, tafiti,
uhaulishaji wa Teknolojia kwa wanafunzi., watafiti na wajasiriamali wa viwanda vidogo na vya kati na dhumuni kubwa la kituo hiki
ni kutoa maarifa shirikishi , kuchochea ubunifu kwa kuunganisha watu wenye fikra na mtazamo sawa ndani na nje ya Chuo cha Sokoine cha Kilimo, lakini
Kwa ujumla kituo hiki kinalenga kujenga bunifu na ujasiriamali kwa kuboresha
mahusiano kati ya chuo, viwanda na taasisi nyingine za nje, "alifafanua Prof.Kashaigili.
Prof. Kashaigili ameongeza kuwa kitengo cha bunifu
kilichoko katika Kurugenzi kitengo cha Sayansi ya Familia na Walaji kilichoko Ndaki ya Kilimo, kinalenga kuboresha bunifu, ujuzi, maarifa na
tafiti zinazosaidia watu kufanya maamuzi yanayolenga ustawi, mahusiano, na rasilimali ili kuweza kufikia maisha bora zaidi.
Aidha Prof. Kashaigili amesema kitengo cha Sayansi ya Familia
na Walaji kinajikita katika maeneo mengi ikiwa ni pamoja na ubunifu na ushonaji
mavazi, mpangilio na upambaji wa ndani ya nyumba pamoja na masuala
yanayohusisha sayansi ya walaji.
"Mafanikio ya viwanda hivi ikiwemo viwanda vya KONGUMO yanategemea
namna viwanda hivi vinavyoweza
kuboresha teknolojia na kujenga uwezo na hatimaye kuzalisha aina nyingi
zaidi za bidhaa za kuuza ndani na nje ya nchi hivyo kuongeza tija na faida kwa
kutumia kiasi kidogo cha mtaji ", alisema Prof.Kashaigili.
Kwa upande wake Mary Masere Mhadhiri na Mbobezi wa masuala ya Ubunifu
wa Mavazi, Utengenezaji wa Samani na Mapambo ya ndani kutoka SUA amesema
kutokana na mchango mkubwa unaotolewa na mafundi nguo nchni katika utengenezaji
wa mavazi, Chuo kupitia washirika wake kimeona kuna haja ya kuwaongezea ujuzi katika
kazi yao ya ubunifu wa mavazi ili iweze kuwa na thamani zaidi.
"Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo
zamani kilikuwa kinajulikana kinahusika na kilimo tu lakini hivi karibuni
kuanzia mwaka 2010 chuo kiliweza kujipambanua na kwenda kwenye Nyanja nyingine
ambazo zinamuhusu zaidi mlaji, sasa kupitia Kitendo cha Sayansi ya Mlaji wakajiweka zaidi kwenye
ubunifu wa mavazi tukitambua mavazi ni kitu muhimu kwa binadamu na tukasema
isiwe tu bora mavazi lakini lazima vazi liwe la ubunifu ili mtu anapovaa muonekano
wake uendane, kwa hiyo kupitia kitengo hiki cha ubunifu tukatambua kuwa kuna
mafundi ambao wanasaidia kushona haya mavazi ndio maana leo tunawapa mafunzo",alisema Mary Masere.
Naye Robert Joseph Mwenyekiti wa KONGUMO la nguo Manispaa ya Morogoro
akizungumza kwa niaba ya washiriki wengine
amesema matarajio yao baada ya mafunzo ni kukakikisha wanafanya ubunifu
wa mavazi wenye tija na wenye kulenga
soko la ndani na nje ya nchi huku akiongeza kuwa mafunzo hayo yatawabadilisha
mafundi katika kutekeleza kazi zao na kuongeza uaminifu kwa wateja.
0 Comments