SUAMEDIA

Utafiti umebaini asilimia 17 ya kaya zinatupa taka ngumu kwenye maeneo madogo na asilimia 70 ya kaya zinahifadhi taka kwenywe madampo ya nyumbani.

 

Na.Vedasto George/Winfrida Nicholaus.

Utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Copenhagen nchini Denmark kupitia Mradi wa Mabadiliko ya Vijiji kuwa Miji RAT, umebaini kuwa asilimia 17 zinatupa taka ngumu kwenye maeneo madogo, huku asilimia 70 ya kaya zinahifadhi taka kwenywe misombo ambayo ni madampo ya nyumbani.



Hayo ya mebainishwa na Dr. Eveline Lazaro ambaye ni Mtafiti Kiongozi wa Mradi wa Ukuwaji wa Vijiji kuwa Miji, ambapo amesema kuwa utafiti huo umefanyika kwa kipindi cha miaka kumi kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Copenhagen cha nchini Denmark, lengo likiwa ni kuangalia changamoto na fursa zilizopo katika ukuaji wa Vijiji kuwa Miji.



Kwa upande wake Prof. Ezron Karimuribo Mkurugenzi wa Uzamili na Utafiti Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA, amesema miji inayoibukia mingine kiholela inabidi ikue, ili iweze kuwa na mamlaka kamili ya miji na iwe na utawala pamoja na muongozo mzuri, na ambao unaendana na matakwa ya nchi.

Naye Dr. Mukuki Hante Mkurugenzi Uendelezaji Miji na Vijiji kutoka ofisi ya Raisi TAMISEMI, amesema kuwa miji inayokua iko zaidi 1454 kwa nchi nzima.

Aidha Prof. Fortunata Makene Mkuu wa Kitengo cha Utafiti Mkakati na Machapisho kutoka taasisi ya Economic and Social Research Foundation ESF, amesema miji imekuwa ikikua kwa kasi kuliko serikali ambavyo imejiandaa katika upangaji wa miji.

Post a Comment

0 Comments